Waziri Mkuu Mizengo Pinda akizungumza katika kilele cha Siku ya Viwanda Afrika katika ukumbi wa PTA sabasaba wakati wa kufunga maonyesho hayo ya siku ya viwanda katika bara la Afrika.

WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Masoko Dakta Abdallah Kigoda amesema kwamba changamoto zilizopo nchini katika sekta ya viwanda kimfumo na zinahitajika kuzipunguza ili kusukuma maendeleo ya kiviwanda nchini.
Akizumgumza katika kilele cha Siku ya Viwanda Afrika, Waziri Dakta Kigoda amesema kwa sasa serikali inatatumia rasilimali fedha za ndani katika kuimarisha ukuaji wa viwanda katika kupambana na tatizo la ajira nchini.
IMG_2105
WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Masoko Dakta Abdallah Kigoda akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya viwanda Afrika jijini Dar.
“Ni dhahiri kuwa, tangu mwaka 1989 pale Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa ulipoazimia kuwa Novemba 20 ya kila mwaka kuwa siku ya viwanda Afrika, imekuwa siku mahsusi kwa wadau kujadili changamoto katika sekta hii muhimu kwa ukuaji wa uchumi,” amesema Kigoda.

Amesema matatizo ya kimfumo ni pamoja na mazingira ya kufanyia biashara, utaratibu wa kuanzisha biashara na uwekezaji na utaratibu wa upatikanaji wa vibali vya ujenzi na utaratibu wa kupata mkopo katika taasisi za fedha.
Dakta kigoda amesema kwamba Tanzania ikiwa miongoni mwa nchi zinazoendelea bado sekta ya viwanda haijaweza kukua kwa kasi ipasavyo ukilinganisha na baadhi ya nchi zinazoendelea barani Afrika.

Amesema Mfano mchache wa mchango wa sekta ya viwanda ni asilimia 40 China, asilimia 16 nchini India, Vietnam asilimia 20 na Tanzania ni asilimia 8.5 tu mpaka sasa.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) Emmanuel Kalenzi amesema ujasiriamali, ajira na maendeleo ya kiviwanda ni jibu pekee katika matatizo ya kijamii na kiuchumi katika bara la Afrika.
Amesema kuwa pamoja na kuhamasisha mambo ya ajira na ujasiriamali katika bara la Afrika lakini bado bara la Afrika lina nafasi ya kusonga mbele na kukuza uchumi wake kwa kujikita zaidi kwenye teknolojia na uwekezaji wenye tija.

IMG_2086
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) Emmanuel Kalenzi akizungumza katika Siku ya Viwanda Afrika.
PG4A2015
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waziri wa Viwanda na Biashara , Dr Abdallah Kigoda wakati alipofunga  maadhimisho ya siku ya  Viwanda Afrika kwenye uwanja wa maonyesho wa Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam.
IMG_2116
Baadhi ya wageni waalikwa kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya Viwanda Afrika jijini Dar.
IMG_2098
Meza kuu.
PG4A2106
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akipata maelezo kuhusu  viatu  kutoka kwa Elizabeth George (kulia)wakati alipotembelea  banda la Woiso Original Products katika maonyesho yaliyoambatana na maadhimisho ya siku ya Viwanda Afrika yaliyofaungwa na Waziri Mkuu kwenye  uwanja wa maonyesho ya biashara ya kimataifa ya Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam . Kushoto kwake ni Waziri wa Viwanda na Biashar, Dr. Abdallah Kigoda na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi. 
PG4A2066
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akipata maelezo kutoka kwa Bw. Gerge Buchafu wa Shirika la  Maendeleo ya Viwanda Vidogovidogo (SIDO)  baada ya kufunga  maadhimisho ya siku ya viwanda  Afrika  kwenye  uwanja  wa Maonyesho wa Mwalimu Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam,  Novemba 20, 2013. Kulia ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Dr. Abdallah Kigoda.
IMG_2138