Afisa
Elimu msingi wilaya ya Sengerema Bw,Juma Mwajombe ilipokuwa akimvua
madaraka Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Luhama kwa kosa la kutotimiza
majukumu yake.
AFISA
Elimu wa Shule za Msingi Sengerema Mkoani Mwanza, Bw Juma Mwajombe
amemvua madaraka Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Luhama iliyoko kata ya
Katwe kwa kushidwa kutekeleza majukumu yake.
Amesema
kuwa amefikia maamuzi hayo kutokana na mwalimu huyo kushindwa kusimamia
vema majukumu yake na kutokusimamia maadili ya walimu wake wanapokuwa
kazini.
Bw,
Mwajombe amemtaja aliy mvua madaraka hayo kuwa ni Mwalimu Maila Majula
baada ya kuchochea ugomvi kati ya mwalimu Emanuel Joely na Mwalimu
Alfonsia Ndalahwa uliosababisha walimu hao kutwangana makonde ofisini
kwa kile kinachodaiwa kuwa walituhumiana kula fedha za ujenzi wa kisima
cha shule hiyo.
Aidha
amesema kuwa Mwalimu Mkuu anapaswa kusimamia vema majukumu yake na
kushauri walimu kuacha migogoro isiyo ya lazima na kuzingatia maadili ya
kazi na siyo kukuza migogoro isiyo ya lazima na kusababisha walimu
kutokuheshimiana sehemu za kazi.
Ameongeza
kuwa baada ya kuona mapungufu hayo ameamua kumvua madaraka hayo na
kuwa mwalimu wa kawaida na kumteua Mwalimu Pema Nteba aliyekuwa mwalimu
mkuu msaidizi katika shule ya msingi Mwangika ilyoko katani humo kuwa
mwalimu mkuu wa shule hiyo,
Wakati
huo huo alimuhamisha Mwalimu Alfonsia Ndalahwa katika shule hiyo na
kumpeka shule ya msingi mwangika .Pia ametoa onyo kwa walimu kuacha
tabia ya kutokuheshimiana kazini badala yake wafuate maadili ya kazi
yao.
0 comments:
Post a Comment