Waziri Mkuu David Cameron asema Somalia imepiga hatua
Mkutano huo unalengo la kumsaidia Rais Hassan Sheikh Mohamud aweze kuijenga tena upya Somalia.
Somalia inahesabiwa kuwa miongoni mwa mataifa yalioanguka na ambayo imekuwa ikihangaishwa na magaidi wa Al shabaab, uharamia na ukame ulioitikisa mwaka kati ya 2010 hadi 2012.
Rais Mohamud wa Somalia amesema serikali yake itafaulu kuidhibiti nchi nzima na kukabiliana na utovu wa usalama ifikapo mwaka 2015.
Mkutano huo utajikita zaidi katika masuala ya kujenga upya vikosi vya ulinzi na kukabiliana na ubakaji ambalo ni suala linalooonekana kama mwiko.
Takriban watu saba waliuawa katika mlipuko wa bomu kwenye gari uliotokea katika mji mkuu Mogadishu siku ya Jumapili. Kundi la Al - Shabab ambalo lina mafungamano na Al - Qaeda linadai kuhusika na shambulio hilo.
Bofya hapa kusoma zaidi
0 comments:
Post a Comment