Maandamano yalifanyika kote duniani kupinga Marekani
Mahakama nchini Misri imewapa hukumu
ya kunyongwa watu saba walioshukiwa kuitengeza filamu iliyosababisha
kero na ghadhabu katika ulimwengu wa kiisilamu mapema mwaka huu.Washukiwa hao saba walihukumiwa wakiwa hawapo mahakamani.
Hukumu hizo ziliidhinishwa na Mufti mkuu nchini Misri ambaye pia ni msomi wa dini ya kiisilamu.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa ni nadra kwa Mufti kupinga hukumu kama hizi.
Filamu hiyo iliyokuwa ya hali ya chini mno, ilitengezwa mjini Carlifonia, Marekani na kutolewa kwenye internet mwezi Septemba.
Miongoni mwa wale walioshtakiwa ni mtengezaji wa filamu yenyewe Morris Sadek ambaye ni raia wa Misri.
Mahakama itatoa hukumu ya mwisho mwezi Januari kufuatia itikio la Mufti
KWA YEYOTE MWENYE KUPENDA TECHNOLOJIA YA COMPUTER
0 comments:
Post a Comment