Mtoto anethy johanes akiwa katika
hospitali ya rufaa mbeya wodi namba 8 anakopatiwa matibabu mtoto huyo
alifikishwa hapo baada ya mama yake mdogo kumchoma moto huku akimlisha kinyesi
ambapo baadaye wasamaria wema walijitokeza kumuokoa mtoto
huyo na baadaye kumpeleka katika hospitali ya rufaa mbeya
.hata hivyo mara baada ya kufikishwa hospitalini hapo madaktari walilazimika
kumkata mkono wake baada ya kile kinachodaiwa kuwa angeweza kupata madhara
zaidi kwa kuwa mkono wake ulianza kuoza.kwa mujibu wa muuguzi wa wodi hiyo
ambaye hakutaka kutajwa jina lake kwa kuwa si msemaji, alisema kuwa hivi sasa
mtoto huyo yuko chini ya uangalizi wa hositali hiyo anahudumiwa matibabu na
kupewa chakula ambapo anapatiwa yai moja na karanga maalumu nyakati za asubuhi
pamoja na chakula.
0 comments:
Post a Comment