TAARIFA YA KIFO CHA MSANII SHARO MILIONEA KUTOKA KWA KAMANDA WA POLISI MKOA WA TANGA
Sharo Milionea enzi za uhai wake
Namkariri Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga Constantine Massawe akizungumza na East Africa Radio jana usiku akisema, “leo majira ya saa mbili usiku kwenye barabara ya Segera Muheza mtu mmoja alietambulika
kwa jina la Hussein Ramadhani au Sharo Milionea akiwa anaendesha gari
namba T478 BVR Toyota Harrier akitokea Dar es salaam kwenda Muheza
alipofika eneo la Maguzonizonga wilayani Muheza hilo gari lake
liliacha njia na kupinduka mara kadhaa na kusababisha kifo chake, mwili
wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza”
Kamanda amesema hakuna kona kali sana wala ubovu wa barabara kwenye
sehemu aliyopata ajali Sharo Milionea, katikati ya Segera na Muheza
ambapo gari imehifadhiwa mahali salama kwa sababu haitembei.
Kwenye gari alikuwa mwenyewe hivyo hakuna taarifa kamili ya nini kilichotokea maana inaweza kuwa alisinzia.
R.I.P Sharo tulikupenda lakini mungu kakupenda zaidi, kazi zako tulizipenda na tutakukumbuka kwa mengi.
Related Product :
Why Shop on Bongo Online?
We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be
0 comments:
Post a Comment