Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, December 18, 2012

Msiwaue wapenzi wa jinsia moja-Museveni.


Rais wa Uganda Yoweri Museveni
Rais wa Uganda Yoweri Museveni

Rais wa Uganda Yoweri Museveni, amesema wapenzi wa jinsia moja hawapaswi kuuawa au kudhalilishwa, huku wabunge wa nchi hiyo wakiendelea na mjadala wa kutathmini kuhusu muswada wenye utata wa kupinga wapenzi wa jinsia moja.
Katika matamshi yake ya kwanza hadharani, kuhusu muswada huo, Rais Museveni amekariri kuwa suala la mapenzi ya jinsia moja halipaswi kupewa nafasi kukita mizizi.
Muswada wa awali uliowasilishwa katika bunge la Uganda, ulipendekeza adhabu ya kifo kwa wale watakaopatikana na hatia ya kushiriki mapenzi ya jinsia moja, lakini kipengele hicho kimefutwa katika muswada mpya.
Katiba ya Uganda kwa sasa inaharamisha mapenzi ya jinsia moja.

Serikali imekana kuhusika na mswada huo

Mwandishi wa Uingereza
Mwandishi wa Uingereza aliyekamatwa kwa kuandika mchezo kuhusu hatma ya wapenzi wa jinsia moja nchini Uganda

Mwandishi wa BBC mjini Kampala, anasema serikali ya nchi hiyo imesema kuwa mswada huo uliwasilishwa na mbunge na wala sio muswada wa serikali.
Katika hotuba yake wakati wa kuapishwa kwa Askofu Mkuu wa kanisa la Anglikana nchini Uganda Rais Museveni, alijiepusha kuupinga au kuunga mkono muswada huo.
Rais alisema, ''ikiwa kuna watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja, hatutawaua au kuwanyanyasa lakini suala la mapenzi ya jinsia moja halipaswi kuhimizwa katika jamii''
''Hatuwezi kukubali mapenzi ya jinsia moja kupewa msisitizo zaidi katika jamii kana kwamba ni jambo nzuri'' aliongeza rais Museveni.
Mawaziri wamewaonya wabunge kuwa ikiwa watapitisha muswada huo, basi kutakuwa na athari kubwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Uganda na jamii ya kimataifa.
Mataifa ya Magharibi yamelaani muswada huo na wametishia kusitisha misaada kwa Uganda ikiwa itapitishwa na bunge la nchi hiyo.
Spika wa bunge la Uganda Bi Rebecca Kadaga amesema muswada huo utapitishwa kama zawadi ya Krismasi kwa mawakili wake.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop