Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Joseph Simbakalia
amewaomba radhi wananchi wa mkoa huo kutokana na kauli Desemba 21, mwaka jana
akiwakebehi baada ya kumwomba apokee maandamano yao ya kupinga mpango wa kusafirisha gesi
hiyo.
Akizungumza katika mkutano wa majumuisho
uliofanyika jana baada ya kusikiliza madai ya wananchi hao kwa siku mbili
mfululizo, Pinda alisema hakuna tone la gesi ghafi itakayosafirisha kwa njia ya
bomba na kusema kiwanda cha kusindika gesi ghafi kitajengwa katika Kijiji cha
Madimba, mkoani humo ili mabaki yatokanayo na gesi hiyo yatumike kuvutia
uwekezaji wa viwanda.
“Wataalamu wanasema gesi haiwezi kwa namna
yoyote ile kusafirishwa kama ilivyo, lazima
ibadilishwe kuwa hewa au barafu… kiwanda cha kusafisha gesi kitajengwa Madimba.
Gesi yote itakayotoka Mnazi
Bay itasafishwa hapo na
masalia yote yatabaki huku ili kuvutia viwanda vya mbolea na vingine
vinavyotumia malighafi hizo,” alisema Pinda na kuongeza:
“Kama tungekuwa tunasafirisha gesi ghafi basi
hata kiwanda cha Dangote kisingejengwa hapa… gesi itakayopelekwa Dar es Salaam ni ile
iliyosafishwa kwa ajili ya matumizi ya kuzalisha umeme… tusaidieni wenzetu
kuliokoa Taifa na tatizo la umeme.”
“Gesi lazima isindikwe Mtwara, haitoki hadi
viwanda vije… nadhani hili ni jambo jema lazima tuliwekee utaratibu.
Nikawauliza wataalamu wangu kwani kiwanda cha kusafisha gesi kinajengwa wapi,
wakanijibu Madimba… nikasema kumbe tatizo kubwa ni kutowaeleza vya kutosha
wananchi suala la gesi.” alisema Waziri Mkuu huku akipigiwa makofi... “Nafikiri
tatizo ni sisi Serikali hatukuwa na mpango mzuri wa kuwaelimisha wananchi.”
Awali, madai ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara
yalikuwa ku pinga usafirishaji wa gesi ghafi kwenda Dar es Salaam wakieleza
kuwa mpango huo utafukuza uwekezaji wa viwanda mkoani humo ambao ungechochewa
na upatikanaji wa malighafi baada ya kusafishwa kwa gesi.
Pia wananchi walipinga uje nzi wa mitambo ya
kuzalisha umeme Kinyerezi, Dar es
Salaam wakiitaka Serikali kujenga mitambo hiyo mkoani
Mtwara.
Alitoa wito kwa wabunge wa Mkoa wa Mtwara kufuta
tofauti zao za kisiasa ili waweze kuharakisha maendeleo ya mkoa huo...
“Purukushani hizi ndani ya chama hazina tija, tuseme basi… wabunge hawaelewani,
sasa bungeni wanakwendaje... kila mtu na lake … hebu tuseme watu kwanza mimi
badaaye,” alisema Pinda huku akishangiliwa.
Katika
siku hizo mbili mkoani Mtwara, Waziri Mkuu alikutana na viongozi wa vyama vya
siasa, dini, wafanyabiashara, madiwani na wenyeviti wa mitaa na wanaharakati
mbalimbali.
MKUU WA
MKOA WA
MTWARA AOMBA RADHI MBELE YA HADHRA KWA KAULI ZAKE
Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa, Simbakalia aliwaomba radhi wakazi wa Mkoa wa Mtwara akisema alipotoka kuwaita wananchi hao wapuuzi na baadaye wahaini kauli ambazo ziliwaudhi wengi
“Kupitia hadhara hii nawaomba radhi kwa
kuwakwaza, nimesikitishwa kwa kauli yangu ambayo imepokewa kwa hisia kwamba
niliwadharau,” alisema Simbakalia.Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa, Simbakalia aliwaomba radhi wakazi wa Mkoa wa Mtwara akisema alipotoka kuwaita wananchi hao wapuuzi na baadaye wahaini kauli ambazo ziliwaudhi wengi
Baadaye Waziri Mkuu aliwasihi wananchi wa Mtwara kumsamehe Mkuu wao wa Mkoa wa Mtwara kwa kauli hiyo aliyoitoa 21 Desemba, mwaka jana katika kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa, (RCC), pale alipoombwa kuyapokea maandamano ya wakazi wa mkoa huo Desemba, 27, mwaka jana.
0 comments:
Post a Comment