Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, January 8, 2013

Wakuu 3 wa polisi wafutwa kazi Kenya


Mkuu wa polisi mkoani Rift Valley John M'mbijiwe anayedaiwa kuwa na uhusiano na mtu huyo mlaghai,John Waiganjo ingawa alikana kumfahamu

Maafisa watatu waandamizi wa polisi nchini Kenya, wamesimamishwa kazi kuhusiana na sakata ya mtu mmoja ambaye aliwalaghai watu kuwa yeye ni naibu kamishna mkuu wa polisi kwa zaidi ya miaka mitano.
Mkuu wa polisi mkoani Rift Valley John M'mbijiwe anayedaiwa kuwa na uhusiano na mtu huyo mlaghai,John Waiganjo ingawa alikana kumfahamu ni mmoja wa wale waliofutwa kazi.
Mwenyekiti wa tume ya kuwaajiri maafisa wa polisi KPSC Johnstone Kavulundi, amesema maafisa hao watatu wametajwa kuhusika kwa njia moja au nyingine na kashfa hiyo.
Wiki iliyopita, Joshua Waiganjo, alifikishwa mahakamani, kwa kujifanya afisa mwandamizi wa polisi katika mkoa wa Rift Valley.
Mshukiwa huyo amekanusha madai hayo.
Ripoti zinasema kuwa ulaghai huo ulifichuliwa, wakati aliposafiri kwa ndege ya polisi, kwenda kuchunguza mauaji wa maafisa 42 wa polisi waliouawa na wezi wa ng'ombe katika bonde la Suguta, tukio ambalo ndilo mbaya zaidi kuwahi kutokea katika historia ya taifa hilo.

Rais Mwai Kibaki ameagiza uchunguzi kamili kuhusiana na tukio hilo.

Bwana Kavulundi amesema kuwa mkuu wa polisi mkoani humo John M'Mbijiwe, afisa mkuu wa kitengo cha polisi cha kupambana na wezi wa mifugo ASTU Remi Ngugi na afisa mkuu wa polisi wilayani Njoro Peter Nthiga wamesimamishwa kazi.
Amesema watatu hao huenda wakahujumu uchunguzi ikiwa wataendelea kusalia madarakani.
Joshua Waiganjo amesemekana kuwafuta kazi na kuwaajiri maafisa wengine wa polisi katika mkoa wa Rift Valley wakati huo.
Baada ya kukana mashtaka hayo, kesi hiyo ilihairishwa ili kumruhusu mshukiwa huyo kutafuta matibabu kutokana na ugonjwa wa kisukari katika hospitali moja nchini humo.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop