Welcome to our online store Portal

Template Information

Friday, February 1, 2013

Jeshi la polisi kilimanjaro lawashikilia watu wawili kwa tuhuma za unyang'anyi wa kutumia silaha


Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Robert Boaz akiwaonesha waandishi wa habari(hawapo pichani)moja ya silaha walizokamatwa nazo watuhumiwa .
Waaandishi wa habari wa Mkoa wa Kilimanjaro wakisikiliza maelezo toka kwa kamanda wa polisi wa mkoa huo Robert Boaz(hayukopichani).
Baadhi ya viongozi waandamizi wa jeshi la polisi mkoa wa Kilimanjaro.
JESHI la polisi mkoani kilimanjaro linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za ujambazi wa kutumia silaha.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro ACP Robert Boaz amewataja watuhumiwa hao kuwa ni, Mohammed Shani (24) na Emmanuel Jumanne (30), wote wakazi wa Bomangombe na Sanya juu wilayani Hai.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kamanda Boaz amesema kuwa januari 19 mwaka huu majira ya saa kumi jioni huko Bomangombe mtuhumiwa wa kwanza Mohammed Shani alikamatwa akituhumiwa kujihusisha na matukio mbali mbali ya unyanganyi kwa kutumia silaha.
Boaz amesema mtuhumiwa huyo alipohojiwa alikiri kuwa anayo silaha ambayo huitumia kwenye matukio mbali mbali ya uhalifu akiwa anashirikiana na wenzake ambapo aliweza kuwaonyesha polisi sehemu alipokuwa ameihifadhi silaha hiyo.
Kamanda Boaz, amesema kuwa silaha iliyokutwa na mtuhumiwa huyo ni, Bunduki aina ya MARK IV ambayo imefutwa namba za usajili na kukatwa kitako na mtutu pamoja na vifaa vya kutendea uhalifu kama kinyago (mask) 1,maboshore 2, masweta 2,pamoja na risasi 13.
Kamanda Boaz, amesema baada ya kuhojiwa, Mtuhumiwa alimtaja alimtaja mtuhumiwa wa pili Emanuel Jumanne na kuelekeza chumba anamoishi na kilipopekuliwa ilipatikana bunduki moja aina ya shortgun iliyotengenezwa kienyeji na risasi mbili za shortgun, kofia ya jeshi la polisi, boshore 1,begi dogo lililokuwa limehifadhia bunduki hiyo.
Aidha kamanda aliongeza kuwa msako ulianza na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo akiwa wilayani Karatu ambapo kwa pamoja walikiri kufanya matukio mbali mbali katika maeneo ya Bomangombe na Sanya juu na Moshi.
Boaz aliongeza kuwa makosa mengine ni madereva wasiokuwa na leseni,ulevi,kutokuwa na motor vehicle licence,kutokuwa na bima na kupakia abiria kwenye magari ya mizigo.
Amesema kiasi hicho cha fedha kimetokana na tozo za notification na lengo kuu likiwa ni kupunguza ajali za vifo na majeruhi.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop