Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema pamoja na baadhi
ya viongozi wa Serikali wakati akiwasili kwenye Ukumbi wa Julius
Nyerere kwa ajili kufungua mkutano wa Majadiliano na Wiki ya Sera za
kuondoa Umaskini, uliofanyika kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere jijini Dar
es Salaam, leo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akisoma hotuba wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Majadiliano wa wiki ya Sera za kuondoa Umaskini, unaoendelea kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo. (Picha na Zainul Mzige).
Taasisi za fedha kwa kushirikiana na Serikali zimetakiwa kubuni mbinu bora za
kuwawezesha wananchi wasiokopesheka ili kuwainua wananchi wa kipato
chini nchini. MOblog inaripoti.
Akizungumza
na wageni waalikwa kwenye ufunguzi wa mkutano wa Majadiliano ya wiki ya
Sera ya kuondoa Umaskini jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais Mhe, Dkt.
Mohammed Gharib Bilal amesema kutokana na sababu mbalmbali, watu
maskini wana nafasi finyu ya kupata fursa na kuzitumia kwa ajili ya
kujiletea maendeleo.
“Katika
suala la kukuza uchumi na kupunguza umaskini, fursa ni nyenzo muhimu
zinazowezesha kufikia malengo. Fursa hizi zinaweza kuwa ni za kisiasa,
kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. Hata hivyo, si watu wote wanaweza
kujua fursa zilizopo,” amesema Dkt. Bilal
Amesema
kuwa kukosekana kwa fursa wanazostahili kuzipata watu masikini kunaweza
kuwa kumesababishwa na sababu nyingi, kama vile za kimazingira, kisera,
kisheria, kiuchumi, kiutawala na kijamii.
Dkt.
Bilal alilisitiza mkutano huo una historia ndefu tangu ulipoanza
kufanyika mwaka 2002 lengo lao limebaki kujikita katika kutoa fursa kwa
wananchi kuchambua na kujadili mafanikio, changamoto na kutafuta
suluhisho lenye kulenga kuyafikia malengo.
“Nitumie
fursa hii kuwakumbusha washiriki wa mkutano huu kuwa, agenda ya kuondoa
umaskini si ya kitaifa pekee, bali ni ya kimataifa. Tangu mwaka 1993,
Umoja wa Mataifa umetenga siku ya tarehe 17 Oktoba ya kila mwaka,”
aliongeza Dkt. Bilal
Amesema
katika harakati za kupambana umasikini Serikali ina programu mbalimbali
kama Dira ya Taifa ya Maendeleo na Mkakati wa Kupunguza Umasikini na
Kukuza Uchumi (MKUKUTA) zenye lengo la kuongeza kasi ya mapambano dhidi
ya umasikini.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Fedha, Mhe Saada Salum amesema mjadala utakuwa wa siku tatu na kauli mbiu “Kupanua wigo katika kutumia mifano bora na fursa zilizopo kwa maendeleo endelevu yenye kunufaisha watu wengi walio maskini’
Amesema
kuwa mijadala mingine ni pamoja na uimarishaji wa sekta ya kilimo,
masuala ya bajeti na umuhimu wake katika kutekeleza miradi na program
zinazogusa maendeleo ya watu na masuala ya hifadhi za jamii.
Kwa Upande wake Afisa Maendeleo Mkuu wa Ubalozi wa Canada na Kaimu Mwenyekiti wa kikundi cha Wadau wa Maendeleo Patricia McCullagh amesema mkutano huo ni fursa ya kipekee kwa wadau wa maendeleo kuzungumzia njinsi ya kuondoa umaskini nchini Tanzania.
Mkurugenzi
Mkazi wa UNDP nchini Tanzania Bw. Phillipe Poinsot akifuatilia hotuba
ya mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (hayupo
pichani).
Naibu
Waziri wa Fedha Mh. Saada Salum akizungumza na wageni waalikwa wakati
wa ufunguzi wa wiki ya kuondoa umasikini jijini Dar es Salaam.
Picha juu na chini ni Afisa Maendeleo Mkuu wa Ubalozi wa Canada na Kaimu Mwenyekiti wa kikundi cha Wadau wa Maendeleo Patricia McCullagh akizungumza
wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wiki ya Sera za kuondoa umasikini
jijini Dar es Salaam ambapo amesema kwamba Tanzania inajukumu la
kusukuma utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuzungumzia vikwazo
ambavyo ni vizingiti vya Maendeleo ya Kiuchumi ya Taifa.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Asasi za Kiraia nchini Tanzania Bw. John Ulanga ambaye
alizungumzia umuhimu wa ushirikishwaji wa Asasi za kiraia katika
mapambano ya kuondoa umaskini.
Baadhi ya wadau wa maendeleo kutoka mashiika ya Umoja wa Mataifa na Taasisi mbalimbali wakifuatilia mkutano huo.
Wadau mbalimbali wa maendeleo wanaohudhuria mkutano huo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKt. Mohammed Gharib Bilal
akibadlishana mawazo na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Lennarth
Hjelmaker, wakati akiondoka kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere baada ya
kufungua rasmi Mkutano wa Majadiliano na Wiki ya Sera za kuondoa
Umaskini, unaoendelea jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment