Mkurugenzi
wa Masoko wa Kampuni ya LG Electronics wa Afrika Mashariki, Moses Marji
(kushoto), Mtafiti katika Idara ya Vijidudu wa Chuo Kikuu cha Sayansi
na Tiba cha Muhimbili (MUHAS), Dk Billy Ngasala na Meneja Masoko wa LG,
Soyoung Lee, wakifungua pazia kuashiria uzinduzi wa viyoyozi vya
kufukuza mbu viitwavyo ‘LG Mosquito Away’ jijini Dar es Salaam leo.
Mtafiti
katika Idara ya Vijidudu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba cha
Muhimbili (MUHAS), Dk Billy Ngasala akihojiwa na waandishi wa habari
muda mfupi baada ya uzinduzi wa viyoyozi vya kufukuza mbu viitwavyo LG
Mosquito Away jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi
wa Masoko wa Kampuni ya LG Electronics wa Afrika Mashariki, Moses Marji
(katikati), Mtafiti katika Idara ya Vijidudu wa Chuo Kikuu cha Sayansi
na Tiba cha Muhimbili (MUHAS), Dk Billy Ngasala (kulia) na Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni ya Alshaaf, Aliraza Rajani wakifanya mahojiano na
waandishi wa habari katika uzinduzi wa LG Mosquito Away jijini Dar es
Salaam leo.
Kampuni
ya vifaa vya teknolojia ya LG Electronics ya Afrika Mashariki leo
imezindua viyoyozi vya kufukuzia mbu iitwayo “LG Mosquito Away” na
katika harakati za kupambana na vimelea vya mbu na ugonjwa wa malaria
nchini
Akizugumza
na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Masoko wa
Kampuni ya LG Electronics, Moses Marji amesema kiyoyozi hicho kipya
kinatoa mawimbi ambayo yanaweza kumfanya mbu kuanguka na kisha kufa
baada ya muda mfupi.
“kifaa
kipya ni kizuri kwa mapumziko ya nyumbani au ofisini na kinampa mteja
nafasi ya kupumzika na kwa maslahi mapana ya kupambana na mbu katika
maambukizi ya ugomjwa wa malaria nchini,” amesema.
Marji
amesema kuwa kifaa hicho kimetengezwa mahsusi kwa mazingira ya Tanzania
na Afrika mashariki kiasi ambacho kitamwezesha Mtanzania wa kawaida
kumudu kununua kwa kujinga na mbu waenezao malaria.
Kwa
upande wake, Mtafiti katika Idara ya Vijidudu wa Chuo kikuu cha Sayansi
na Tiba Cha Muhimbili (MUHAS), Dakta Billy Ngasala amesema baada ya
utafiti juu ya wadudu wa malaria ndipo wakashirikiana na LG kuja na
mbinu mpya ya kumuangamiza mbu hapa nchini.
Amesema
kwamba taasisi ya MUHAS kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani
(WHO) kwa viwango vyao walifanya utafiti Bagamoyo kwa mbu ili
kubadilisha mbinu ya kupambana mbu na kudhibiti ugonjwa wa malaria.
“tulifanya
utafiti juu ya ugonjwa wa malaria na jinsi ya kudhibiti ugonjwa wa
malaria katika harakati za kupambana na maambukizi ya ugonjwa huo ili
kuja na mbinu mbadala badala ya dawa peke yake,” alisisitiza.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Alshaaf Bargain Centre,
Ali Raza kwamba bei ya kiyoyozi ni kwa mujibu wa soko la Tanzania na
Afrika Mashariki kwa ujumla.
Amesema
kuwa kiyoyozi kimetengezwa kwa kumlenga Mtanzania na kwa mazingira ya
nchi ni nafuu kwa matumizi na rahisi kutumia kwa watu wote.
0 comments:
Post a Comment