Baadhi
ya wanafunzi wakipita na mabango yenye ujumbe mbalimbali mbele ya
Jukwaa Kuu, wakati Makamu alipokuwa akipokea maandamano hayo kwenye
maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, katika Viwanja vya Mnazi Mmoja,
jijini Dar es Salaam, leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati
wa Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, kwenye Viwanja vya
Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi Mpango Mkakati wa 3 wa Kitaifa
wa Kudhibiti Ukimwi (NMSF3), wakati wa sherehe za Maadhimisho ya Siku ya
Ukimwi Duniani, zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar
es Salaam, leo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dkt. Seif Rashid, (wa pili kulia) ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam, Mwantum Mahiza, Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya kudhibiti Ukimwi
Tanzania, Dkt. Fatma Mrisho.
Makamu wa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi mija
kati ya Vitabu vya Mkakati wa 3 wa Kitaifa wa Kudhibiti Ukimwi (NMSF3),
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Alhad Mussa, baada ya ya kuzindua
mpango mkakati huo wakati wa sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi
Duniani, zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es
Salaam, leo.
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata
utepe kuashiria kukabidhi rasmi, Mashine za CD4 kwa ajili ya Kanda za
Juu Kusini, wakati wa sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani,
zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza
maelezo kutoka kwa Meneja wa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwai, chini
ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Angela Ramadhan, wakati
alipokuwa akitembelea Mabanda ya maonyesho katika Maadhimisho ya Siku ya
Ukimwi Duniani, yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar
es Salaam, leo. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mwantum
Mahiza, Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya kudhibiti Ukimwi Tanzania, Dkt.
Fatma Mrisho.
Makamu wa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahi na mtoto
Samir Isagetee (miezi 7) akiwa na Mama yake, Lilian Amani,
wakati alipotembelea katika Banda la Watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi
NACOPHA, katika Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, zilizofanyika
leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam. Mtoto huyo ni
mmoja kati ya watoto waliozaliwa na wazazi wenye maambukizi ya Virusi
vya Ukimwi na yeye kuzaliwa salama.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea mabanda katika maadhimisho hayo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha
ya pamoja na baadhi ya viongozi.
0 comments:
Post a Comment