Serikali imekiri mfumo wa ulipaji kodi na ule wa utumiaji wa mashine za kutolea risiti(EFDs) kuwa ni mbovu na hivyo unahitaji kufanyiwa kazi.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda,
amesema mfumo wa ulipaji kodi nchini bado unakabiliwa na matatizo
ambayo hayawezi kusaidia katika kumuendeleza mfanyabiashara zaidi ya
kumkandamiza.
Dk Kigoda alisema hayo wakati alipokutana na
wafanyabiashara wa mikoa yote nchini, kuhusu maboresho katika ukusanyaji
wa mapato yatokanayo na kodi na tozo mbalimbali wanazotozwa
wafanyabiashara, wajasiriamali na mapendekezo ya uendeshaji wa biashara
nchini.
Alisema baada ya serikali kulitambua hilo hivi
sasa inajipanga kutafuta ufumbuzi utakaosaidia kumaliza changamoto hizo.
Hata hivyo, bado kuna kazi kubwa ya kupata mfumo bora wa uendeshaji
biashara na ulipaji kodi.
“Suala la mashine za kutolea stakabadhi
mmelizungumzia kwa mapana, lakini hata hivyo bado zina changamoto lakini
haya yote mliyoyazungumza wakati nikienda kukutana na wenzangu
endeleeni na kufanya biashara zenu kwa utaratibu wenu wa zamani hadi
ufumbuzi utakapatikana,” alisema Dk Kigoda.
Dk Kigoda alisema kama mtakumbuka kuna taarifa
zilizowahi kutolewa na vyombo vya habari kimataifa kuwa Tanzania ilikuwa
ni moja ya nchi iliyofanya vibaya katika kipindi cha mwaka jana
kutokana mfumo mbaya uliosbabishwa na sababu mbalimbali ikiwamo masuala
ya ukusanyaji kodi.
Aidha, aliwataka kuwa wavumilivu wakati matatizo
yao yakishughulikiwa kwani watambue matatizo ya kiuchumi hayatatuliwi
kwa migomo, maandamano ya kisiasa bali hutatuliwa kiuchumi.
“Tanzania tuna tatizo kubwa sana na lazima
tuliondoe hili siyo lingine bali ni kutoaminiana kati ya serikali na
wafanyabiashara. Hili lazima tulitatue kwa sababu serikali tunaona
wafanyabiashara ni wajanja wanaweza kukwepa kodi wakati wafanyabiashara
nao hivyo hivyo….” alisema na kuongeza:
Huku akishindwa kuweka wazi akiepuka kulizungumzia
kwa undani suala la EFD, zaidi akiwapongeza wafanyabiashara hao kwa
kauli yao kuwa hawapingi kulipa ko.iN Aliwasihi suala hilo litakwisha
baada ya kikosi kazi kitakachoundwa kikiwashirikisha wafanyabiashara
hao.
“Hatuwezi kumkamua ng’ombe atoe maziwa bila kumpa
majani na hatuwezi kumaliza matatizo ya uchumi kwa maandamano au
kuwasikiliza wanasiasa. Njia pekee ya kutatua matatizo haya ni
kushirikisha wataalamu wa uchumi” aliongeza.
Dk Kigoda alisema waraka uliotolewa na
wafanyabiashara utafanyiwa kazi na haki itatolewa baina ya
mfanyabiashara mkubwa, wa kati na mfanyabiashara mdogo
Alisema serikali itaunda kikosi kazi
kitakachoshirikisha jumuiya hiyo ya wafanyabiashara ili waweze kuwekeza
katika mazingira mazuri.
Dk Kigoda alisema kupitia utaratibu huo ni vyema wakaangalia
mfumo wa ulipaji kodi uwe ni mfumo unaoendeleza biashara na sio mfumo
unaotoa kodi ili zitumike.
“Kupitia utaratibu huu ni vyema tukaangalia mfumo
wa ulipaji kodi uwe ni mfumo wa kuendeleza kodi na sio kulipa kodi ili
tutumie na kwamba hapa tutakaa kikao na wenzangu na wa TRA na Wizara ya
Fedha na baada ya hapo tutatoa tamko”alisema Dk Kigoda na kuongeza
“Nawahakikishia mimi kama waziri mwenye dhamana ya
viwanda na biashara lengo langu kubwa ni kusukuma serikali katika
punguza gharama za biashara kwa wafanyabiashara na changamoto yetu hii
ya utumiaji wa mashine hizi tutamaliza kupitia taratibu za
kiuchumi”alisema
Katika hatua nyingine, Waziri Kigoda
Waziri Kigoda amewatetea wafanyabiashara wadogo
manaofanya baishara zao katika maduka ya Kariakoo kwa kusema kuwa
wanachangia pato la taifa katika kukuza uchumi.
“Wafanyabaishara wadogo ndio wanaochangia pato la
taifa katika kukuza uchumi wa nchi tofauti na wafanyabaishara hao
wakubwa na hata hivyo wafanyabaishara hao wakubwa walianzia kama hao
wafanyabiashara wadogo”aliongeza.
Pia amewakalipia askari wanaofanya doria katika
soko la Karikaoo maarufu kama “Tigo” kutoka na wafanyabaishara hao kudai
kuwa askari hao wamekuwa tishio kwa kuwakamata bila kufauata utaratibu.
Mwakilishi kutoka Zanzibar
Mwakilishi kutoka Zanzibar Lacky Zahoor alisema
tatizo kubwa ni ulipaji wa kodi katika nchi hiyo kwamba huko Zanzibar
mashine hizo hwazihitaji kwa sababu zina tunza kumbukumbu zao sio hasara
zao.
“Sisi tupo tayari kulipa kodi lakini mfumo
uboreshwe uwe mzuri kwa ni hizi mashine kwetu Zanzibar hatuzitaki kwa
sababu hazionyeshi hasara tunayopata sisi zaidi ya kumbukumbu zao tu
hivyo hatuzikubali”alisema Zahoorn
Mshauri wa Jumuiya wafanyabiashara wa Kariakoo,
Johnson Minja alisema chimbuko linaloonekana kuwa mzigo kwa
wafanyabiashara hao ni kitendo cha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),
kuingia katika awamu ya pili ya utumiaji wa mashine hizo za kukusanyia
kodi, bila kufanya tathimini ya kutosha juu mafanikio na changamoto
zilizojitokeza wakati wa awamu ya kwanza ya utumiaji mashine hizo
Baadhi ya maduka katika soko la Kariakoo jana yalifungwa
kutokana na wafanyabiashara hao kuhudhuria mkutano na kusababisha
usumbufu kwa wateja waliofika eneo hilo la Kariako kwa ajili ya manunuzi
ya bidhaa mbalimbali.
Hata hivyo wafanyabiashara hao walitofautiana
kwani kwa upande wa wafanyabiashara wa maduka ya nguo wengi wao
hawakufungua huku wa vifaa vingine kama vya ujenzi walifungua maduka.
Wakizungumza jana kwa nyakati tofauti baadhi ya
wafanyabiashara waliuofungua maduka walisema kuwa wenzao wengi
hawajafungua kutokana na kushiriki katika mkutano.
Rehema Ahmed mmoja wa wafanyabiashara hao alisema
kuwa viongozi wao waliwataka wasifunge maduka lakini kutokana na mkutano
huo kuwa na umuhimu waliamua wengi wao kufunga maduka.
Mkutano huo ulihudhuriwa na zaidi ya
wafanyabiashara 3500 kutoka kila kona ya nchi ikiwemo wa wakilishi
kutoka Tanzania Visiwani.
Wafanyabiashara hao walianza kuwasili majira ya
saa tatu na nusu asubuhi huku waziri wa Viwanda na biashara akiwaziri
katika ukumbi huo saa 5:15 asubuhi.
Wafanyabaishara hao walikuwa na vipeperushi vilivyokuwa vimeandikwa “Kodi bila mashine inawezekana
0 comments:
Post a Comment