Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na viongozi wa wilaya ya Kiteto baada
ya kuwasili wilayani humo Januari 16, 2014 kufuatilia suala la mauaji
ya wakulima. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wanakijiji wa Mtanzania Januari 16,
2013 wakati alipokwenda kuwapa pole kufuatia uvamizi waliofanyiwa na
watu wanaosadikiwa kuwa wafugaji ambao waliua watu watatu na kuchoma
nyumba . Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Erasto Mbwilo.
Baadhi
ya wananchi wa Kiteto wakimsikiliza Waziri Mkuu , Mizengo Pinda
wakati alipowahutubia Januari 16, 2014 katika mji wa Kibaya alipokwenda
kuwapa pole wakulima wa wilaya hiyo ambao walishambuliwa, kuuwawa na
nyumba zao kuchomwa moto na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafugaji.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akiagana na wazee wa Kiteto wakati alipoteta nao
baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika mji mdogo wa Kibaya
Janauari 16, 2014. Alikwenda Kiteto kuwapa pole wakulima ambao
walishambuliwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafugaji ambao waliua na
kuchoma moto nyumba.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
0 comments:
Post a Comment