Welcome to our online store Portal

Template Information

Sunday, January 26, 2014

WAZIRI APONEA CHUPU CHUPU JALI YA NDEGE

http://azizicompdoc.blogspot.com/

Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar, Abubakari Khamis Bakar, abiria na marubani wawili wamenusurika kifo baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria kupata ajali.
Waziri Bakar pamoja na abiria wapatao 17 walipata ajali hiyo kisiwani Pemba jana baada ya breki za ndege hiyo ya Shirika la Ndege la ‘ZANZ AIR’ kushindwa kufanya kazi, muda mfupi baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume, nje kidogo ya Mji wa Chakechake, Mkoa wa Kusini Pemba.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, baada ya ndege hiyo kutua ikitokea Unguja, ilikwenda kwa kasi na walitarajia ingepunguza mwendo kama ilivyo kawaida, lakini ilishindwa kufanya hivyo.
Walieleza kushtushwa na ndege hiyo iliyokuwa ikiendelea kwenda kasi mfano wa gari la mashindano, hali iliyomlazimu mwongoza ndege aliyekuwa akijiandaa kuiongoza kuikwepa kwa kukimbilia kando ya uwanja huo kunusuru maisha yake.
Meneja wa uwanja huo Rajabu Ali Mussa, alisema: “Ni kweli, tukio hilo lilitokea saa 10:30 jioni baada ya ndege hiyo kupata hitilafu ya kiufundi. Uchunguzi wa awali ulionyesha chanzo cha ajali ni kufeli kwa breki zake.”
Aliongeza: “Ni kweli jana ndege hiyo ya ‘ZAN AIR’ ilipata hitilafu na kuingia kwenye nyasi, lakini baadaye abiria wote waliokuwemo na marubani wake wawili, walitoka salama.’’
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Saleh Mohamed Saleh alisema tangu jana jeshi hilo, limeimarisha ulinzi kuzunguka eneo la uwanja, ili kulinda ndege hiyo.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop