Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, March 4, 2014

CHAMA KIPYA CHA ACT CHAVUNA VIONGOZI WA CHADEMA


http://azizicompdoc.blogspot.com/

Chama kipya cha siasa cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania) kimeanzishwa na kupewa usajili wa muda huku kikitamba kuwa mbadala wa vyama vyote vilivyopo sasa kwa maelezo kuwa vimekosa demokrasia ya kweli.
Miongoni mwa viongozi wa muda wa chama hicho ni Samson Mwigamba aliyetimuliwa uanachama wa Chadema kutokana na kuhusishwa na waraka uliotaka kumwandaa Zitto Kabwe kuwania uenyekiti wa chama hicho.
Mwigamba aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, alitimuliwa pamoja na aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo, huku uanachama wa Zitto aliyevuliwa nyadhifa zake zote zikiwamo za Naibu Katibu Mkuu na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, ukisubiri kesi aliyofungua mahakamani.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwigamba alisema mchakato wa kuandikisha wanachama mikoani kwa ajili ya kuomba usajili wa kudumu kwa mujibu wa sheria umeshakamilika.
Alisema kimepata wanachama katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar. Hata hivyo, alisema kimechagua mikoa 10 ambayo Msajili wa Vyama vya Siasa atakwenda kuhakiki kama sheria inavyoeleza kabla ya kupewa usajili wa kudumu.
“Kama tutafanikiwa kupata usajili wa kudumu mapema, tunatarajia kushiriki kwa nguvu zote katika chaguzi zote ndogo zitakazojitokeza, uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu mwakani,” alisema Mwigamba.
Alisema bendera ya chama hicho itakuwa na rangi ya zambarau inayoashiria haki, heshima na uadilifu na rangi nyeupe inayonyesha uwazi na usafi.
“Katikati ya bendera inayozungukwa na rangi zambarau kuna nyota mfano wa chama kinachojitokeza katikati ya vyama vingi inayokuja kutatua matatizo ya wanyonge yaliyowakabili kwa kipindi kirefu,” alisema Mwigamba na kuongeza:
“Pembeni mwa bendera hiyo kuna misitari ya rangi ya dhahabu inayoonyesha rasilimali zetu, rangi nyeusi zinazoashiria sisi ni Waafirika.”
Alisema hivi sasa hakuna kiingilio katika kujiunga na chama hicho na kwamba mara baada ya kupatikana kwa katiba, ndipo suala hilo litakaposhughulikiwa sambamba na kiingilio.
Mwenyekiti wa chama hicho, Kadawi Limbu alisema ACT - Tanzania kinaamini katika demokrasia jamii na kina shabaha kuu ya kupigania na kusimamia mabadiliko na uwazi ambayo ni lazima jamii inufaike nayo.

Alisema ACT-Tanzania kinaongozwa na msingi mitano ambayo ni: uzalendo, usawa, uadilifu, demokrasia ya kweli, uwazi na uwajibikaji vitu ambavyo vyama vyote vya siasa nchini vimeshindwa kuvisimamia kwa vitendo.
“Hakuna chama hata kimoja chenye demokrasia ya kweli na hii inatokana na vyama kuanzishwa na watu kwa malengo yao. ACT-Tanzania inakuja kuwafuta machozi wanyonge wote kwani vyama 21 vilivyopo vimeshindwa,” alisema Limbu aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance For Democratic Change (ADC) na kuongeza:
“Watu wameipora demokrasia, wanyonge wanahangaika kutafuta usawa katika huduma za jamii kama elimu, afya na nyinginezo. Sisi hatutakubali, tutahimiza usawa kwa kila kitu.”
Msajili wa Vyama vya Siasa, Francis Mutungi alithibitisha chama hicho kupata usajili wa muda na kusema kipo katika hatua za kusaka usajili wa kudumu.

Alisema ACT-Tanzania kinaongozwa na msingi mitano ambayo ni: uzalendo, usawa, uadilifu, demokrasia ya kweli, uwazi na uwajibikaji vitu ambavyo vyama vyote vya siasa nchini vimeshindwa kuvisimamia kwa vitendo.
“Hakuna chama hata kimoja chenye demokrasia ya kweli na hii inatokana na vyama kuanzishwa na watu kwa malengo yao. ACT-Tanzania inakuja kuwafuta machozi wanyonge wote kwani vyama 21 vilivyopo vimeshindwa,” alisema Limbu aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance For Democratic Change (ADC) na kuongeza:
“Watu wameipora demokrasia, wanyonge wanahangaika kutafuta usawa katika huduma za jamii kama elimu, afya na nyinginezo. Sisi hatutakubali, tutahimiza usawa kwa kila kitu.”
Msajili wa Vyama vya Siasa, Francis Mutungi alithibitisha chama hicho kupata usajili wa muda na kusema kipo katika hatua za kusaka usajili wa kudumu.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop