Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, March 18, 2014

SERIKALI TATU KUONGOZA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Jaji Sinde Warioba leo aweka wazi kwanini tume yake ilipendekeza serikali tatu kwa nia ya kudumisha muungano pamoja na changamoto kutokosekana ila kuna uwezo mkubwa wa kuondoa kero nyingi za muungano na kudumisha muungano wetu, suala la ukubwa na uzito wa serikali hizo amesema ni suala la kawaida na sio zito kama linavyofikiriwa na wengi ktk nchi, uthubutu lazima uwepo tukitaka kuishi bila migongano ktk muungano wetu.
Katika kuielezea Zanzibar kuhusu changamoto za muungano amesema kiuhalisia huwezi kuikataza leo znz isiitwe nchi na wakati katiba ya nchi hiyo inatambua kama nzn ni nchi kamili ktk muungano wa nchi mbili yaani Jamhuri ya watu wa Zanzibar na Jamhuri ya watu wa Tanganyika. Mamlaka ya viongozi wa nchi ya znz yalionekana kuchukuliwa na Rais wa muungano na baadae kurudishwa kupitia katiba mpya ya Zanzibar, kitu ambacho kwa sasa ni kigumu kutokana na sheria zinazotungwa na bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania kuonekana hazitatumika znz mpaka baraza la wawakilishi znz litakapozipitia na kuzipitisha sheria hizo.

Mgawanyo wa mapato ya muungano umekua mgumu na kusababisha mapato ya muungano kutumika zaidi ktk upande mmoja wa muungano ambako ni Tanzania bara. Akaunti ya pamoja ni miongozi mwa mambo ya makubaliano ktk muungano lakini limekua gumu mpaka sasa kufanyiwa kazi, Mamlaka ya waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano ni mpaka zanzibar, lakini haonekani waziri mkuu kukagua miradi ya maendeleo zanzibar, halikadhalika kwa rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania haonekani kufanya hivyo kwa zanzibar.
Suala la Tanganyika kujificha ktk koti la muungano limedhihirishwa dhahir leo bungeni na Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba Jaji Sinde Warioba na kuwaasa wajumbe wa bunge hilo kua makini na maamuzi yao ili kufikia mafanikio mazuri ya kudumisha muungano wetu na kusema ye na wajumbe wenzake wametoa pendekeze la kua na serikali tatu badala ya mbili za sasa kama inavyotambua katiba yetu.

Rasimu hiyo imeonyesha kuvuta hisia za wajumbe wengi wa bunge maalum na kutoa ahadi za kufanya vizuri zaidi ktk maamuzi yao kama alivyotoa shukrani zake makamu mwenyekiti wa bunge maalum Mh Samia Suluhu. Mungu ibariki Tanzania, mungu ibariki Afrika

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop