Welcome to our online store Portal

Template Information

Thursday, March 6, 2014

SIRI NZITO YAIBUKWA KUHUSU IPTL

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Maswali juu ya utaratibu uliotumika kutoa fedha zilizokuwa zimewekwa kwenye Akaunti ya Escrow katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kutokana na mvutano baina ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na IPTL yameanza kupata majibu.
Wakati mmiliki kwa Kampuni ya VIP Engineering and Marketing, James Rugemalira ameibuka na kukiri kuwa yeye ni miongoni mwa waliolipwa fedha hizo huku uongozi wa IPTL ukifafanua utata kuhusu mkataba wake na Tanesco na jinsi kampuni hiyo ilivyouzwa jumla kwa Pan African Energy.
Katika ufafanuzi wake, Rugemalira alisema kati ya fedha zilizokuwa katika Akaunti ya Escrow, yeye akiwa mwanahisa wa IPTL alilipwa Dola za Marekani 75 milioni (Sh120 bilioni), alizoziita ‘vijipesa vya ugoro’ sawa na asilimia 30.
Alisema baada ya kuuza hisa zake kwa Kampuni ya Pan African Power (PAP) aliruhusu pia asilimia 70 ya hisa za mbia mwenzake, Mechmar kutoka Malaysia ziuzwe pia kwa PAP.
Alisema kwenye akaunti hiyo kulikuwapo na Dola za Marekani 120 milioni, tofauti na kiwango kilichotajwa na Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu aliyesema fedha hizo zilikuwa Dola 122 milioni.
Rugemalira alisema pia kuwa hatua ya kufikiwa kwa hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na Jaji John Utamwa Januari 17, mwaka 2014 saa 8: 30 usiku, ilitokana na Waziri wa Nishati kumuomba wamalize kesi zilizokuwa mahakamani.
“Niliiambia Serikali kuwa nyie mmeibiwa na sisi tumeibiwa. Mimi nikawaambia kuwa ‘the end justify the means’ (jambo la muhimu ni matokeo, si njia ulikopitia), mwisho tulikubaliana kwamba kwa masilahi ya Taifa tumalize kesi hii, na mimi ndiyo nikalipwa hivyo vijipesa vya ugoro,” alisema Rugemalira.
Hatua ya kutoa fedha zilizokuwa kwenye Akaunti ya Escrow na kugawiwa kwa VIP Engineering na PAP, imefikiwa huku mkopeshaji wa IPTL, Benki ya Standard Charted ya Hong Kong (SCB-HK), inayodai Dola za Marekani 145 milioni (Sh234.456 bilioni), ikiwa haijalipwa na wala haijajulikana italipwa kwa kutumia kanuni gani.
Itakumbukwa kuwa, baada ya benki za Malaysia zilizokuwa zimeikopesha IPTL kuyumba kiuchumi, deni la benki hizo lilinunuliwa na SCB-HK.
“Tumeridhia kuwa hizo asilimia 70 zichukuliwe na PAP na Standard Charted anadai kwamba yeye ndiye mkopeshaji na dhamana yake ni hiyo mitambo, kitu ambacho siyo kweli. Lakini kama ni kweli aende mahakamani kuthibitisha,” alisema Rugemalira.
Hukumu iliyotolewa Februari 12, 2014 na Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji cha Washington DC, Marekani, ilitaka pande hizo mbili zikae na kukubaliana namna ya kukokotoa gharama ambazo shirika hilo la umeme linapaswa kuilipa benki hiyo.

Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa habari jana, Rugemalira alionekana kujikanganya juu ya kuitambua SCB-HK, kuna wakati alisema haitambui na hivyo haikuwa na fedha zilizokuwa Escrow na wakati mwingine alisema bado anaidai benki hiyo na kesi ipo mahakamani.
Rugemalira alisema kwamba alikuwa Mkurugenzi wa IPTL hadi Januari 24, mwaka huu alipong’atuka, ingawa pia alisema baada ya kung’atuka alikuwa bado anaiwakilisha IPTL kwenye vitu vingi, ikiwa ni pamoja na kuuza hisa zake kwa PAP.
Katika mkutano huo wa waandishi wa habari, Rugemalira alitumia muda mrefu kuipigia debe PAP akisema ni kampuni bora inayoweza kuzalisha umeme kwa bei nafuu.
“Swali la kujiuliza sasa, IPTL ni nani, jibu lake ni PAP,” alisema Rugemalira.
Pia kuhusu suala la Mkataba wa IPTL na Tanesco kuanza 1995 na kutarajiwa kufikia kikomo 2015, Rugemalira alisema siyo sahihi na kuwa mkataba huo ulianza 2002 na ulitarajiwa kukamilika 2022.
Akizungumzia suala hilo, Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh alisema kwa sasa hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa bado hana taarifa rasmi.
“Kwa sasa siwezi kusema chochote, hizi taarifa ndiyo kwanza nazisoma, lakini kama itagundulika kuna vitu vimekiukwa, kuna vyombo husika vitakavyochukua hatua,” alisema Utouh.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita), Philip Saliboko alisema ofisi yake ilikabidhiwa kazi ya ufilisi wa IPTL na Mahakama mwaka 2008 lakini mahakama hiyohiyo iliamuru Rita inyang’anywe ufilisi huo, Septemba 5, mwaka jana.
Saliboko alisema baada ya kunyang’anywa mamlaka ya ufilisi, IPTL ilikabidhiwa kwa Kampuni ya Pan African Energy Ltd (PAT) iliyoelezwa kuinunua.
“Hata hivyo, ofisi yangu haikupewa ufilisi wa muda mrefu, ilipewa wa muda mfupi, kwa hiyo majukumu yangu hayakufikia yale ya kuuza au kufilisi mitambo, bali kuuangalia kama IPTL ipo salama hadi hatua nyingine zitakapotajwa,” alisema.

Mwanasheria wa IPTL, Joseph Mwakandege alisema PAT ilinunua hisa kutoka kwa VIP Engineering na Nechmar kwa uwiano wa asilimia 70 kwa 30 na baada ya kununuliwa hisa hizo, Mahakama iliamuru kuwa PAT iwe mbia wa jumla wa Kampuni ya IPTL.
Mwakandege alipohojiwa kuhusu mkanganyiko wa mkataba kati ya Serikali na IPTL, alisema makubaliano baina ya pande hizo yalikuwa ni yale ya Kujenga, Kuendesha na Kumiliki (BOO), hivyo mali za IPTL zinabaki kuwa zake hadi baada ya mkataba kumalizika 2015.
Alisema mkataba huo haukuwa na kipengele cha kuiachia Serikali mitambo yake ya kuzalisha umeme.
Kuhusu Akaunti ya Escrow, mwanasheria huyo alisema haikuwa akaunti ya Serikali, bali fedha zilizokuwamo zilikuwa mali ya IPTL baada ya kuwapo kwa mgogoro baina ya wadau – IPTL na Tanesco.
“Kwanza ifahamike kuwa Escrow ilianzishwa kwa ajili ya wadau. Baada ya VIP Engineering na Nechmar kuuza hisa, akaunti ilikabidhiwa kwa PAT,” alisema.
Alisema baada ya mgogoro huo kutokea, kila mdau aligawiwa kiasi chake cha hisa na kuondoka, hivyo fedha zilizobaki ni za IPTL.
Alikanusha kuwa Akaunti ya Escrow ilikuwa na Dola za Marekani 270 milioni, bali Dola 105 milioni na wala si zaidi ya hapo.
“Nyinyi mnafikiri Escrow ni ya Serikali. Mnafikiri Serikali ni wajinga na mafisadi kiasi hicho?” alisema.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop