Welcome to our online store Portal

Template Information

New Products
Showing posts with label Mbowe. Show all posts
Showing posts with label Mbowe. Show all posts

Thursday, January 16, 2014

MBOWE KUMSHITAKI ZITTO KABWE,

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), amesema anamsubiri Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe mahakamani.

Zitto ametoa kauli hiyo siku moja baada ya Mbowe kutangaza kumburuza mahakamani, kutokana na kile kinachodaiwa kumzushia tuhuma za uongo. “Nasema sitaki malumbano na kiongozi yeyote, nachotambua masuala ya mahakamani yanajibiwa mahakamani na si vinginevyo,” alisema Zitto.
Zitto alitoa kauli hiyo, baada ya azizicompdoc.blogspot.com kutaka kujua msimamo wake kutokana na kauli ya Mbowe kukusudia kumshitaki, kutokana na madai ya kusema uongo dhidi yake.

 Zitto ambaye yuko nchini Nigeria anakohudhuria vikao vya Kamati za Bunge za Hesabu za Serikali kwa nchi za Afrika, alisema pamoja na hali hiyo, mahakama ndiyo njia pekee ambayo haki ya mtu inaweza kupatikana.
Alisema kwa msingi huo, hivi sasa hayuko tayari kuruhusu malumbano ambayo hayana tija kwa taifa.
 “Nipo Nigeria na bahati mbaya ninaumwa sana, ila hivi leo ninamshukuru Mungu nimepata nafuu kidogo. Kama nilivyosema mwanzo sitaki malumbano na mtu.
 Pamoja na kusema anaumwa, hakuwa tayari kufafanua ni ugonjwa gani unaomsumbua.

 “Huu muda nahitaji kutafakari maisha yangu kisiasa na kwa vyovyote vile masuala ya mahakamani yatajibiwa mahakamani,” alisisitiza Zitto.

 Juzi Kurugenzi ya Habari na Uenezi ya CHADEMA, ilitoa taarifa kwa vyombo vya habari na kusema, Mbowe amezushiwa tuhuma zisizokuwa na ukweli wowote, zikilenga kumchafua kwa nafasi yake ya uongozi na kuipaka matope taasisi anayoiongoza.

 Kutokana na hali hiyo, tayari Mbowe kwa mujibu wa taarifa hiyo, ameshawasiliana na wanasheria wake kwa ajili ya kuchukua hatua za kisheria dhidi ya aliyezusha uongo huo.

 Ingawa taarifa hiyo haikutaja jina la Zitto, lakini hivi karibuni mbunge huyo katika ukurasa wake wa facebook, aliibua tuhuma nzito dhidi ya Mbowe.

 Zitto, Samson Mwigamba na Dk. Kitila Mkumbo, walivuliwa nyadhifa zao na Kamati Kuu (CC).  

Baadaye CC iliwatimua uanachama, Mwigamba na Kitila kwa tuhuma za kukisaliti na kukihujumu chama, huku Zitto akikimbilia mahakamani kuzuia asijadiliwe.  

Katika tuhuma hizo, Zitto alidai Mbowe alipokea michango ya fedha kutoka kwa makada wa CCM, Nimrod Mkono na Rostam Aziz, kusaidia kampeni za CHADEMA mwaka 2005 na 2010.  

Pia Zitto, alidai Mbowe alipokea Sh milioni 40 mwaka 2005 kutoka kwa Mkono ili asifanye kampeni katika Jimbo la Musoma Vijijini, na kwamba mwaka 2008 alimpatia Sh milioni 20 kusaidia CHADEMA ishinde uchaguzi mdogo wa Tarime. 
Kutokana na tuhuma hizo, CHADEMA kupitia Ofisa Habari Mwandamizi, Tumaini Makene, iliamua kujibu mapigo. 
Katika taarifa hiyo, ilieleza tuhuma hizo ni moja ya mikakati ya Zitto na wenzake wanaotaka kuhamisha mjadala wa makosa yanayowaandama ya utovu wa maadili na usaliti dhidi ya chama.

 “Hivi karibuni, Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe, amezushiwa tuhuma zisizokuwa na ukweli wowote, zikilenga kumchafua kwa nafasi yake. 
“Tuhuma hizo ni pamoja na kwamba, Mbowe mwaka 2005 eti alichukua fedha kutoka kwa Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono kiasi cha Sh milioni 40 ili Mbowe asifanye kampeni katika jimbo hilo.  

“Mwaka 2008, Mbunge Mkono alimpatia Mbowe Sh milioni 20 kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa Tarime, kisha akazitoa kwenye chama kama mkopo na akalipwa.” 
Zitto alidai mwaka 2010, wakati wa uchaguzi mkuu Mkono alimpatia Mbowe Sh milioni 200 kwa ajili ya kampeni za mgombea urais, huku akipokea Sh milioni 100 kutoka kwa Rostam. Kutokana na hali hiyo, Idara ya Habari ya CHADEMA, ilisema kupitia taarifa yake kuwa hakuna ukweli hata mmoja katika tuhuma hizo, bali ni uongo na uzushi uliopangiliwa kama moja ya mikakati ya watu wenye malengo ya kutaka kuilaghai jamii kwamba viongozi wa CHADEMA hawana tofauti na wale wa CCM. 
View detail

Thursday, December 19, 2013

MBOWE KITANZINI MATUMIZI MABAYA YA PESA ZA WATANZANIA

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Wabunge jana waliumbuana kuhusu matumizi mabaya ya fedha za umma huku Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe akituhumiwa kuagiza kubadilishwa kwa tiketi ya ndege ya Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Joyce Mukya ili afupishe ziara yake ya kikazi huko Marekani na kwenda Uarabuni kwa shughuli binafsi.

Mbali ya Mbowe, Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi (CCM) anadaiwa kuchukua posho ya Kamati ya Hesabu za Bunge (PAC), kwa safari ya kwenda Dubai na wenzake lakini badala yake akaenda Mbeya kwenye ziara za chama chake.
Malumbano hayo yaliibuka jana baada ya Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba (CCM), kuomba mwongozo wa Spika akitaka kufahamu kauli ya ofisi yake kwa Mbowe kutumia nafasi yake kumrudisha mbunge ambaye ameshatumia fedha za Serikali.
Alidai kwamba Mbowe aliagiza Mukya aanze safari Desemba Mosi, mwaka huu kutoka New York, Marekani ili aende Dubai, Falme za Kiarabu (UAE) kabla ya kwenda Dar es Salaam, Desemba 3, mwaka huu.
Alipoulizwa kuhusu tuhuma hizo jana, Mbowe alisema hawezi kuzungumza chochote kwa kuwa hakuwapo bungeni akisema alikuwa Dar es Salaam kwenye kikao.... “Siwezi kusema lolote mpaka nipate hansard (kumbukumbu rasmi ya Bunge) na kutoka kwa wabunge wangu walioko Dodoma kujua nini kimesemwa.”
Akiomba mwongozo Nchemba ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM alisema: “Jambo hili limechukua taswira kama ni Bunge lote linafanya mambo haya na limevunja heshima ya Bunge. Jambo hili linatuvunjia heshima hata watu ambao tuna maadili ya uongozi na tunaliheshimu taifa letu...
“Pamoja na kuwa jambo hilo lilikuwa la binafsi, lakini kuna ujumbe tumeupata kuwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani amemzuia mbunge wake kusafiri na magazeti yakaandika kwamba wana mahusiano. Mimi sipendi kwenda kwenye uhusiano, nataka kwenye taswira ya Bunge na Taifa.”
Alisema Bunge linapopanga safari za wabunge linazingatia wa chama tawala na wapinzani ili kuweka uwakilishi.
Nchemba alisema Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, aliandika ujumbe mfupi wa simu kwa mtumishi mmoja wa Bunge akitaka kubadilishwa kwa tiketi ya ndege ya mbunge.
Aliusoma ujumbe huo: “Rejea mazungumzo yetu bwana Kabunju kuhusu mheshimiwa Joyce Mukya ambaye yupo safarini. Nitashukuru kama utambadilishia booking (safari) yake ili aweze kurudi, aondoke New York tarehe moja Desemba na kurejea Dubai baadaye ataunganisha kurejea Dar es Salaam by Mbowe kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni nakala kwa Joyce Mukya.” Kabunju S. Kabunju ni Ofisa wa Bunge anayeshughulikia masuala ya usafiri.
Nchemba alisema: “Ameshakatiwa tiketi, ameziba nafasi ya kwenda kuliwakilisha taifa kule, anamwita arudi Dubai na ni mbunge viti maalumu. Je, hili lina taswira gani kwa taifa na kiti chako kinatoa kauli gani kwa watu ambao wanakwenda kutumia fedha za Serikali kwa mambo binafsi, Dubai?” alisema.
Pia alitaka kufahamu Bunge linachukua hatua gani stahiki kwa mbunge anapoingilia kazi za kiti na pia watumishi wanapoingiliwa na kubadilisha yale waliyotumwa kwa ajili ya Serikali.
Mbunge wa Mbozi Magharibi (Chadema), David Silinde alisema Nchemba anaegemea zaidi wabunge wa upinzani wakati wapo wa CCM waliochukua posho.
“Mheshimiwa Mwenyekiti, yaliyosemwa na magazeti na mwombaji wa mwisho (Nchemba), alipokuwa anatoa mwongozo amejaribu kuainisha wabunge wa upande mmoja wa upinzani,” alisema.
Alimtaja Zambi kuwa alichukua fedha ili kwenda Dubai na wenzake lakini badala yake alikwenda Mbeya wakati Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipokuwa katika ziara mkoani humo. Zambi pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya.
“Tunaomba mwongozo wako namna gani hili suala litachukuliwa hatua na wala siyo kufanya propaganda za kisiasa ndani ya Bunge lako,” alisema Silinde.
Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Mariam Msabaha alisema kuna mambo mengi yanayofanyika ndani ya Bunge hilo lakini hayasemwi.
“Kuna watu wameandikwa ndani ya magazeti wanaiba vidani licha ya kutosemwa lakini imeonekanika huku. Mambo ya mapenzi ni ya mtu na mtu wake, humu kila mtu ana mpenzi wake,” alisema.
Mwenyekiti wa PAC na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe alisema: “Kamati ya PAC ambayo inahusika na masuala ya fedha za umma tayari imeshamwomba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), afanye uchunguzi kuhusiana na safari zote ili jambo hili liweze kufika mwisho.”
Alisema taarifa hiyo itapelekwa kwa Spika na kama atapendezwa italetwa bungeni ili jambo hilo liweze kumalizika.
Akijibu mwongozo huo, Mwenyekiti wa Bunge aliyekuwa akiongoza shughuli za jana asubuhi, Mussa Azzan Zungu alisema: “Nimepokea miongozo yote na kiti kinasema hakina lazima ya kujibu sasa hivi, kitatoa mwongozo baada ya kufikiria na kuyatafakari hapo kitakapopata nafasi.”
Hata hivyo, kabla ya kuahirisha Bunge jana mchana, Zungu alisema suala hilo ni la kiutawala na masuala yote yanayohusu masuala ya fedha yanatawaliwa na sheria na kanuni za fedha.
Sakata hilo liliibuliwa bungeni wiki iliyopita na Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally Keissy alipokuwa akichangia taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (Laac).
View detail

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop