Welcome to our online store Portal

Template Information

New Products
Showing posts with label Serikali. Show all posts
Showing posts with label Serikali. Show all posts

Thursday, December 19, 2013

SHERIA YA KUDHIBITI UHALIFU KTK MTANDAO KUTUNGWA


cyber 01
Mkurugenzi wa TEHAMA  wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  Dkt. Ally Simba akimkaribisha mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Patrick Makungu (hayupo pichani)  katika ufunguzi  wa kongamano la siku mbili kuhusu sheria  ya mtandao jijini Dar es Salaam.
cyber 02
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  Profesa Patrick Makungu akifafanua jambo wakati akifungua kongamano la siku mbili kuhusu sheria ya mtandao ambalo limeshirikisha wadau mbalimbali wa mtandao, kongamano hilo limefanyika jijini Dar es Salaam.
cyber 03
Baadhi ya wadau wakimsikiliza kwa makini Mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Patrick Makungu (hayupo pichani) wakati akifungua kongamano la siku mbili kuhusu sheria  ya mtandao jijini Dar es Salaam.
cyber 04
Mtoa mada wa kwanza katika kongamano la siku mbili kuhusu sheria  ya mtandao Bw. Said Kalunde akitoa mada iliyohusu uhalifu wa mtandao jijini Dar es Salaam.
cyber 05
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini kongamano la siku mbili kuhusu sheria  ya mtandao jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Eliphace Marwa – Maelezo).

Serikali yaendelea kushirikisha wadau mbalimbali wa mitandao ili kuweza kupata sheria itakayosimamia matumizi  salama ya mitandao hapa nchini.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kongamano la siku mbili jijini Dar es Salaam mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Patrick Makungu alisema kuwa serikali inashirikiana na wadau mbalimbali nchini na nje ya nchi kwa lengo la kupata maoni yao.
“Kongamano hili linakutanisha wadau muhimu ambao maoni yao yataweza kufanikisha kupatikana kwa sheria ya mtandao ambayo itakuwa ndiyo suluhisho la uhalifu wa mtandao ambao unaonekana kushamiri sana hapa nchini na duniani kwa ujumla,” alisema Profesa Makungu.

Aidha Profesa Makungu aliongeza kuwa katika kupambana na uhalifu wa mtandao Tanzania imeandaa miswada mitatu ya sheria ya usalama wa mtandao  ambayo pia inatumika katika Shirikisho la Maendeleo Kusini mwa Afrika(SADC).
“Sheria hizo ni sheria ya mtandao, sheria ya usalama wa taarifa na sheria ya biashara mtandao kwa kufanya hivi tuko sambamba na Jumuiya ya afrika Mashariki, Shirikisho la Maendeleo Kusini mwa Afrika na Umoja wa Afrika ambao wote wana lengo moja la kupambana na uhalifu wa mtandao,” aliongeza Profesa Makungu.

Naye Mkurugenzi wa TEHAMA toka Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  Dkt. Ally Simba alisema kuwa kama hakuna  sheria ya mtandao ni rahisi uhalifu wa mtandao kupunguza wawekezaji  kwani usalama wa fedha unakuwa ni mdogo.
Serikali inaendelea  kukusanya  maoni ya wadau mbalimbali kuhusu sheria ya mtandao kwani mchakato wa kupata sheria uko katika hatua za mwisho na ambapo mwakani  katika miezi ya mwanzoni sheria hii itakuwa tayari.
View detail

Sunday, November 17, 2013

SERIKALI YA TANZANIA YACHARUKA KUHUSU KUCHUKUA HISA ZA KILA MGODI TANZANIA

IMG_2438
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amesema kwamba kuanzia sasa hakuna mgodi utakaoanzishwa bila ya serikali kuwa na hisa.
Kauli hiyo imetolewa leo na  Profesa Muhongo wakati wa  utiaji  saini hivi karibuni katika makubaliano ya kukabidhi mgodi wa dhahabu wa Tulawaka kwa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kutoka kwa Kampuni ya Uchimbaji wa Madini  ya Afrikan Barrick  Gold (ABG) katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo jijini Dares Salaam.
Utiaji saini huo ulifanywa na Mkurugenzi Mkuu wa  STAMICO, Gray  Mwakalukwa  na Makamu wa Rais wa  ABG, Deo  Mwanyika.

 “STAMICO   itachimba katika mgodi huo kwa niaba ya Watanzania, hivyo serikali  itaiwezesha kiutendaji, kifedha,kiutalaamu  na kuwa na rasimali watu, amesema Profesa Muhongo.
 Aliongeza kuwa baadaye   shirika hilo  litauza hisa  kwa Watanzania.   
Amesema STAMICO imenunua mgodi huo kwa dola za Marekani milioni 4.5, ambapo kati ya fedha dola milioni 3.5 zimeshalipwa moja kwa moja.
Akizungumzia kuhusu uuzaji wa mgodi huo, Mwanyika  amesema  kulingana na sera zao uchimbaji huo hautakuwa na faida  kwao , hivyo eneo hilo  linafaa kuendelezwa na  wachimbaji wa kati.

 Amesema STAMICO itachukua mdogi huo na baaadhi ya leseni za utafutaji wa madini zinazozunguka eneo hilo kwa gharama hiyo na kukubali kutoa asilimia 2 ya mrabaha iwapo uzalishaji utazidi wakia 500,000 zikiwa na kikomo cha dola za Marekani 500,000.
 Mwanyika alifafanua kwamba STAMICO itachukua umiliki na usimamizi wa mfuko wa fedha za ukarabati wa mazingira ikiwa kama sehemu ya mpango wa ufungaji wa mgodi huo na itakuwa na dhamana ya majukumu yaliyopita na ya baadae yanayohusiana na kufunga mgodi na ukarabati wa mazingira.

 Aidha itawajibika kulipa fidia kwa wahusika wengine wa mkataba huo iwapo majukumu yao yalioainishwa hayakutekelezwa na ABG itailipa STAMICO salio lililobakia kwenye mfuko wa kukarabati mazingira ambayo kwa sasa ni dola za Marekani milioni 17.6,ambapo bei pia ya mauzo kwenye makubaliano itapunguzwa kutoka kwenye salio.
Katika hatua nyingine Profesa Muhongo amesema  watu wenye maeneo makubwa ya  vitalu  vya madini  ambayo hawajayafanyia kazi  yatachukuliwa kulingana na Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na watapewa wachimbaji wadogo.

Amesema STAMICO itakuwa inawasimamia wachimbaji wadogo, itawasaidia kupata mikopo kiurahisi kutoka Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB), kutoa elimu ya uchimbaji na kuhifadhi mazingira kupitia vyama vyao.
View detail

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop