Welcome to our online store Portal

Template Information

Thursday, December 6, 2012

BABU WA LOLIONDO JELA MIAKA 7

Mchungaji Ambilikile Masapile ‘Babu Ambi’ wa Samunge, Loliondo, Arusha, atapanda kizimbani kukabili kesi za madai na jinai, hii ni kwa mujibu wa wakili maarufu, Mabere Nyaucho Marando.
Wakili huyo alisema, endapo mahakama itamkuta na hatia ya kutenda jinai, Babu Ambi, anaweza kuhukumiwa kifungo kisichopungua miaka saba jela.
Marando alisema, kesi ya jinai ambayo Babu Ambi anafunguliwa ni ile ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kwamba aliwahadaa watu kuwa dawa yake inatibu, wakati hakuna mtumiaji aliyepona.
Aliongeza kuwa kesi ya madai, inafunguliwa kwa sababu anatakiwa alipe fidia za watu waliopoteza maisha na wote waliosafiri kutokana sehemu mbalimbali wakitumia gharama kubwa kwa dawa isiyotibu.
Marando alifafanua, Babu Ambi, anaweza kukumbana na kifungo hicho endapo atakutwa na hatia kutokana na sheria ya jinai namba 302.
“Nipo makini na suala hili, hawezi kupona, nitasimamia kesi na tutamfunga,” alisema Marando na kuongeza:
“Nina taarifa nyingi kuhusu watu waliokufa, hakuna aliyepona.
Mazingira ya kisheria, yanatoa picha rahisi kuwa Babu atakutwa na hatia.”
Kutokana na msimamo huo, Marando aliwataka wale wote waliotibiwa na Babu Ambi lakini hawakupona, waende kwake kwa sababu amedhamiria kuisimamia kesi hiyo.
“Kiukweli babu aliwadanganya watu kuwa anatibu magonjwa sugu, lakini watu walipokwenda na kupata kikombe, hawakupona, na hawezi kuthibitisha mahakamani kuwa dawa yake imethibitishwa na serikali kuwa inatibu magonjwa aliyoyasema,” alisema Marando.
Aliongeza kuwa yupo tayari kuandaa kesi hizo na ndugu wote waliokunywa dawa na hawakupona, wanaweza kwenda kwake ili wakusanye ushahidi wa kutosha.
“Ni jambo linaloumiza, nitasimamia kesi hiyo na nitahakikisha anafungwa si chini ya miaka saba kama sheria inavyosema...ama zake ama zetu, alisababisha wagonjwa wa Ukimwi kuacha kutumia ARV, wengine wakatoroka hospitalini kwenda kwake na wengi wamepoteza maisha,” alisema Marando.
Wakili huyo aliigeukia serikali na kuilaumu kwa kumruhusu Babu kuwapa dawa watu wakati ikijua kuwa ilikuwa haijafanyiwa majaribio ya kitaalamu kujua kuwa kama inatibu au la.
Alisema anaweza kumfungulia kesi ya madai mchungaji huyo kwa kuwa wagonjwa wengi waliuza mali au kuchukua akiba zao na kusafiri hadi Samunge wakijua kuwa watapona baada ya kunywa dawa yake.
“Badala ya kupona wengi walifariki dunia huku wengine wakibaki masikini na hawajapona kutokana na udanganyifu mkubwa uliofanywa na Babu huyo na sasa hawawezi tena kupata mali nyingine,” alisema Marando.
Mwanasheria mwingine, Dk. Ngali Maita alipohojiwa kwa simu alisema atakuwa tayari kumsaidia mawazo ya kisheria Marando ikiwa atahitajika kwa kile alichodai, Babu alidanganya watu kuhusu tiba ya kikombe.
“Ni kitu kibaya sana alifanya Babu wa Loliondo, amesababisha maafa makubwa kwa jamii na mbaya zaidi hadi sasa uchunguzi wa dawa yake upo gizani, serikali haisemi chochote licha ya kuahidi wananchi kuwa watataarifiwa… hii ni mbaya na ni hatari,” alisema Dk. Ngali.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop