Waziri mkuu wa zamani wa Mali Cheick Modibo Diarra
Mataifa mbalimbali duniani yameghadhabishwa na jeshi
la Mali kwa kumkamata na kumlazimisha waziri Mkuu wa nchi hiyo Cheick
Modibo Diarra kujiuzulu.
Marekani imesema kukamtwa kwa bwana Cheick Modibo Diarra ni pigo kwa utawala wa kidemokrasi nchini Mali.
Kadhalika Umoja wa Mataifa umeitishia kuiwekea Mali vikwazo nayo serikali ya Ufaransa iimesema kuwa panahitajika jeshi ambalo litakaloleta uthabiti katika taifa hilo.
Rais wa Mali sasa amemteua Django Sissoko kuwa waziri Mku mpya.
Tofauti na Jeshi, Bwana Diarra alikuwa amependekeza kuhusisha jeshi la Afrika Magharibi ili kukabiliana na wapiganaji wa kiislamu wanaodhibiti sehemu ya kaskazini.
0 comments:
Post a Comment