Wapinzani na wafuasi wa Rais wa Misri Mohammed Morsi kwa sasa wanafanya mikutano mikubwa kabla ya sehemu ya kwanza ya kura ya maamuzi itakayofanyika Jumamosi.
Wapiga kura wataamua kuhusu rasimu ya katiba mpya ambayo inaungwa mkono na waislamu wakijumuisha Rais Morsi. Wapinzani wanasema rasimu hiyo imeandikwa vibaya.
Wameikashifu wakisema kuwa Rais anajaribu kuipitisha rasimu hiyo bila kufanya mashauriano yanayohitajika.
Kura hiyo ya maamuzi itasimamiwa na Idara ya Mahakama lakini majajii wengi wanasema kuwa watasusia shughuli hiyo.
Rais wa nchi hiyo Mohammed Morsi anasisitiza kuwa katiba inastahili kukamilisha kipindi cha mpito kutoka kwa utawala wa Hosni Mubarak
Utata huu umeibua maandamano makubwa nchini Misri pamoja na ghasia kutokea ndani na nje ya mji wa Alexandria.
'Ushindi wa kiisilamu'
Rais Morsi, pia amelipa jeshi mamlaka ya kuwakamata raia huku akisababisha wasiwasi kuwa Misri inarejea katika utawala wa kidikteta.
Sauti za Misri: Kura ya maoni
Hali ya usalama hata hivyo haijazuia ghasia kati ya makundi hasimu katika mji wa bandarini wa Alexandria.Mamia walipigana kwa kurushiana mawe na silaha zengine. Magari kadhaa yalichomwa huku watu kadhaa wakijeruhiwa.
Ghasia zilitokea baada ya mhubiri mmoja kuwataka waumini kupigia rasimu hiyo kura ya ndio
0 comments:
Post a Comment