Afisaa mmoja mkuu nchini China ameachishwa kazi
kufuatia madai kuwa alivunja sheria ya ya ndoa ya nchi pamoja na sheria
ya kuruhusiwa tu kuwa na mtoto mmoja.
Inaarifiwa kuwa afisaa huyo, Li Junwen alivunja sheria kwa kuwa na wake wanne na watoto kumi.Vyombo vya habari vya serikali vinasema kuwa bwana, Li Junwen, alipata watoto wanne na mke wake wa kwanza na tayari alikuwa ameishi na wanawake wengine watatu ambao alipata nao watoto waliosalia.
China inaruhusu tu wazazi kuwa na mtoto mmoja la sivyo walipe faini kwa serikali kila mtoto wa ziada.
Inajulikana kuwa wanawake wengi nchini China hulazimishwa kutoa kimba zao wanapojulikana kuwa na mbimba ya pili.
Mwandishi wa China Ma Jian aliyeandika kitabu kinachoelezea mateso wanayopitia wanawake wa China chini ya sheria ya mtoto mmoja
0 comments:
Post a Comment