Welcome to our online store Portal

Template Information

Thursday, December 27, 2012

Wafuasi wa Morsi watoa wito wa umoja

Maandamano nchini Misri
Raia wa Misri wakiandamana

Wafuasi wa rais wa Mirsi Mohammed Morsi, wametoa wito kwa raia wote wa Misri, kushirikiana baada ya katiba mpya yenye utata kuidhinishwa.
Kiongozi wa chama cha Muslim Brotherhood, Mohammed Badie, amesema raia wote wa Misiri, wazee kwa kina mama, Wakristo na Waislamu ni sharti waanza mikakati ya kuujenga upya taifa lao, kwa hiari.
Zaidi ya asilimia sitini ya watu waliopiga kura wakati wa kura ya maamuzi waliunga mkono katiba hiyo, licha ya kuwa ni asilimia thelathini ya wapiga kura wote walishiriki katika zoezi hilo.
Wakosoaji wanasema, katiba hiyo mpya inawapendelea Waislamu na inahujumu azma na nia ya mageuzi ya kisiasa nchini humo.
Rais Hosni Mubarak, aliondolewa madarakani Februari mwaka wa 2011, baada ya kuwa uongozini kwa takriban miaka thelathini.
Baada ya kutolewa kwa matokeo ya kura hiyo ya maoni hiyo jana, mamia ya wapinzani wa katiba hiyo walifunga daraja moja katika mji mkuu Cairo huku wakiteketeza magurudumu ya magari na kukatiza shughuli za usafiri katika barabara hiyo.
Wafuasi wa chama cha Muslim Brotherhood
Wafuasi wa chama cha Muslim Brotherhood baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kura ya maoni

Uchaguzi wa bunge nchini humo sasa utafanyika katika miezi miwili ijayo.
Mgawanyiko ulioibuka baada ya kura hiyo ya maoni, umesababisha msukosuko wa kiuchumi na kuna ripoti kuwa raia wengi sasa wakibadilisha fedha zao na kuwa na dola za Kimarekani.
Kuna ripoti kuwa kuna uhaba mkubwa wa sarafu ya dola katika maduka ya forodha.
Kabla ya matokeo hiyo kutangazwa serikali ya nchi hiyo ilitangaza kuwa watu wanaotoka au kuingia nchini humo wataruhusiwa kubeba dola lefu kumi pekee kila mmoja.
Siku ya Jumatatu, benki kuu nchini humo ilitoa taarifa kuwa, ina hazina ya kutosha ya sarafu za kigeni kukithi mahitaji ya wote.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop