Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, January 22, 2013

Ufaransa yazidiwa nchini Mali Uingereza yajitosa kuisaidia

Hali yawa tete kwa serikali ya Ufaransa nchini Mali. Serikali ya Uingereza inatarajiwa kujadili mpango wa kutoa msaada zaidi kwa wanajeshi wa Ufaransa wanaopambana na waasi nchini Mali.
Wanajeshi wa Mali wampokea msaada kutoka kwa Ufaransa na sasa Uingereza inataka pia kuwasaidia

Serikali ya Uingereza inatarajiwa kujadili mpango wa kutoa msaada zaidi kwa wanajeshi wa Ufaransa wanaopambana na waasi nchini Mali.
Waziri mkuu David Cameron, amesema kuwa huenda msaada za usafiri na kijasusi ukatolewa kwa wanajeshi hao. Ndege mbili za kijeshi tayari zimetolewa kwa jeshi la Ufaransa.
Waziri wa ulinzi anasema kuwa hakuna mipango ya kufanya mashambuli ya ardhini kwa sasa.
Kuhusu vifo vya raia wa Uingereza katika mashambulizi kwenye kiwanda cha gesi nchini Algeria yaliyofanywa na wapiganaji wa kiisilamu, bwana Cameron alisema kuwa eneo la Kaskazini mwa Afrika linageuka kuwa ngome ya wapiganaji wa kiisilamu.
Wasiwasi kuhusu athari za kundi la kigaidi la al-Qaeda katika ukanda huo, zinaonekana kudhibitiwa kufuatia mpango wa kuwapeleka wanajeshi wa Ufaransa kupambana na wapiganai wenye uhusiano na Al Qaeeda nchini Mali na Algeria ambako waliwateka nyara wafanyakazi wa kigeni.
Wanamgambo waliowashambulia wafanyakazi wa kigeni nchini Algeria, ambapo takriban mateka 48 waliuawa wametoa wito kwa Ufaransa kusitisha harakati zao nchini Mali.

Waiziri mkuu alisema kuwa Uingereza pamoja na washirika wake wako katika mapambano dhidi ya kasumba ambayo inatia doa kubwa dini ya kiisilamu na ambayo inaamini kuwa mauaji na ugaidi yanakubalika na tena ni sharti yafanyike.
Jibu la jamii ya kimataifa kwa tisho hili liitakuwa swala muhimu katika ajenda ya mkutano wa nchi nane zilizostawi duniani G8.
"lazima tupambane na hao magaidi kwa kutumia mbinu zote za kuweka usalama. Lazima tuwakomeshe, kijeshi. Ni lazima tuzungumzie hii kasumba yao, sharti tufunge hii nafasi wanayoitumia, kuendesha harakati,zao'' alisema waziri mkuu.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop