Welcome to our online store Portal

Template Information

Monday, February 4, 2013

MBUNGE WA MTWARA MJINI AWEKWA KIKAANGONI

Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mtwara kimedai kauli zilizotolewa na mbunge wake jimbo la Mtwara mjini, Hasnain Murji kuungana na wananchi wanaoshinikiza gesi kutotoka mkoani humo kwenda Dar es Salaam, ni sawa na kukihujumu chama.
Akizungumza na gazeti hili jana Katibu wa CCM mkoani humo, Alhaji Masoud Mbengula alisema chama kilishangazwa na kauli za mbunge huyo, kwa mba alionekana wazi kuwaunga mkono wapinzani na siyo wananchi.
“Tayari tumemwita katika vikao na kumhoji kuhusiana na kauli alizozitoa, pia taarifa rasmi zipo na tumezipeleka makao makuu ya chama ambapo ndiyo watatoa uamuzi,” alisema Mbengula na kuongeza;
“Tumesikitishwa sana na kauli ya Murji. Kauli yake ilionekana kuwaunga mkono wapinzani kwa kuwa msimamo na nia yao ni kuona Ilani ya CCM haitekelezwi. Kama alikuwa na hoja alitakiwa kutafuta njia za kusema na siyo kuzungumza jambo hilo hadharani. Kwa namna moja au nyingine yeye amechangia kukihujumu chama.”
Wakati katibu huyo akieleza hayo, Desemba 29 mwaka jana baada ya Murji kutoonekana kwenye maandamano ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara ya kupinga gesi kupelekwa Dar es Salaam yaliyofanyika Desemba 27, aliibuka na kusema anaunga mkono wananchi hao kutetea maslahi yao.

Alisema hoja ya msingi ni kujadili kwa namna gani bomba la gesi litanufaisha Wanamtwara, kufafanua kuwa kwa kiasi fulani hakubaliani na hoja ya gesi isiende Dar es Salaam lakini naungana na wananchi kudai jinsi watakavyonufaika na gesi hiyo.
Alisema anakubalina na gesi iende Dar es Salaam kwa sharti la kuzalisha umeme, si kwa matumizi mengine, kwamba wakianza kuitumia kwenye viwanda watakuwa wameiua Mtwara kabisa, huku akiunga mkono wana nchi kuandamana kwa maaelezo kuwa ni haki yao ya msingi na hawapaswi kubezwa na mtu yeyote kwa sababu wanateteta haki yao ya msingi ya kufaidika na rasilimali yao.
Katika maelezo yake Mbengula alisema chama hicho kilihujumiwa huku akitoa mfano wa matukio ya kuchoma moto nyumba. Nyumba hizo nyingi zilikuwa za viongozi wa CCM wakiwamo wabunge pamoja na ofisi, hasa zipo zilizochomwa wilayani Masasi mkoani humo.
“Nyumba zilizochomwa moto zote ni za viongozi na wabunge wa CCM. Mpango huu ulionekana kupangwa na kuratibiwa na watu fulani kwa lengo la kukihujumu chama” alisema Mbengula.
Murji 
azizicompdoc.blogspot.com Jumapili jana lilizungumza na Murji ambapo pamoja na mambo mengine alisema kuwa kauli alizozitoa nazo ziliungwa mkono na CCM.
“Hata siku moja zikuwahi ku pinga gesi kwenda Dar es Salaam.Lengo langu ni kutaka wananchi wafaidike kwanza na gesi, watu walitaka kujua watanufaika vipi na si vinginevyo,” alisema Murji na kuongeza;
“Hata katika ufafanuzi alioutoa Waziri Mkuu alieleza jambo hilo, hata CCM waliungana na mimi kutaka gesi iwanufaishe wakazi wa Mtwara.”
Alisema kuwa kwa sasa hali imekuwa shwari mkoani humo, huku akiwataka wananchi kuwa watulivu, kwani tayari Serikali imeshaeleza msimamo wake na jinsi itakavyotekeleza mradi huo.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop