Welcome to our online store Portal

Template Information

Monday, February 11, 2013

WAZIRI MEMBE AKAGUA UJENZI WA KIWANDA CHA SARUJI LINDI

Mkuu wa wilaya ya lindi Dr Hamidi Nassoro wa kwanza kushoto akiwa Waziri wa 
Mambo ya nje Bernard Membe (wapili kushoto akikagua maendeleo ya ujenzi wa 
Kiwanda Cha Cement Mkoani Lindi leo, ambako Kiwanda hicho kinajengwa 
na kutarajiwa kutoa ajira kwa zaidi ya watu 600.



Akipewa maelekezo na wasimamizi wa mradi huo na kampuni inayojenga

 
Waziri Membe Akiangalia vifaa vitakavyotumika kwenye ujenzi.


Magari na vifaa mbalimbali vikiendelea na kazi ya maandalizi ya ujenziwa kiwanda.
  
Vifaa vya kutosha kwenye eneo hilo vinaonekana huku kukiwa na vijana zaidi ya 280 wakiwa wamepata ajira za muda.

Baadhi ya vifaa kazi kwenye eneo hilo linalotarajiwa kuwa kiwanda  kikubwa cha cement.  
Takriban Wakazi 600 wa Manispaa ya Lindi watanufaika na Ajira mara  utakapokamilika Ujenzi wa Kiwanda cha Simenti kilichoanza hatua za awali za Ujenzi wake huku Tayari zaidi watu 260 wakiwa wamepata ajira katika hatua za awali baada ya kuanza kwa kazi hiyo hivi karibuni Akizungumza na Wakazi wa Manispaa ya Lindi mara baada ya kukagua kazi za Ujenzi wa kiwanda hicho kilichoanza ujenzi kufuatia Upatikanaji wa Gesikatika Mikoa ya Lindi na Mtwara,
 Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe alitoa wito kwa Wazazi na walezi kuongeza jitihada za kusomesha watoto wao ili wanufaikena ajira zitakazopatikana kutokana Uwepo wa Viwanda na shughuli mbalimbali zinazotokana na Gesi ikiwemo Upanuzi wa Bandari ya mji wa Lindi. Waziri Membe alitembelea kukagua kazi za ujenzi wa Kiwanda hichoMaeneo ya Machole Manispaa ya Lindi ambapo alielezwa kazi inavyoendelea na ajira zilizopo kwa sasa Sambamba na Gesi ya Mtwara,Waziri Membe alibainisha kuwa Kampuni ya Satoil ya Norway tayari imegundua uwepo wa Gesi nyingi umbali wa Km 85 baharini kutoka manispaa ya Lindi na kupatikana kwa gesi hiyo,Serikali tayari Imeshaingia mikataba ya Uchimbaji wake Gesi hiyo iliyogunduliwa na kampuni ya Satoil itasaidia maendeleo ya Lindi kwa kuwa kutajengwa kiwanda cha Mbolea,Kiwanda cha vifaa vya plastiki aina zote pamoja na Upatikanaji wa uhakika wa nishati ya Umeme alimalizia Membe kwa kusema Lindi Kucheleeeee!!!! 

Awali akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake,Meneja Mradi wa Lindi Cement kiwanda ambacho kinajengwa na Kampuni ya Meis Industries,Bw Valerian Magembe alibainisha kuwa kazi ya Ujenzi wa kiwanda hicho itakamilika na kuanza Uzalishaji June 2014 ambapo zaidi ya wananchi 600 watanufaika na Ajira na kueleza kuwa kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 500 kwa siku Ndg Waandishi mipango yetu iko vema kama mnavyoona kazi inavyoendelea na tayari Maji na Umeme ndio tunakamilisha,,Wana Lindi wakae mkao wakula kwa kupata ajira na ongezeko la pato la kila mdau kwa sekta yake Na pia nawahakikishia kiwanda hiki ni cha kisasa na hakutokuwa na uharibifu wa Mazingira kutakuwa na mtambo wa kudhibiti Vumbi Tumejipanga vilivyo Alimalizia Bw Magembe Kazi za Ujenzi wa kiwanda hicho kinachomilikiwa na Kampuni ya Wazawa ya Meis Industries kinatarajiwa kuzalisha tani 500 kwa siku kitakapokamilika huku tayari ajira zaidi ya 280 zimetolewa kwa wakazi wa mji huo kwa awamu ya kwanza ya kazi za Ujenzi

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop