28% YA WANAFUNZI WAMEAMBUKIZWA HIV AFRICA YA KUSINI
wasichana waambukizwa Ukimwi nchini SA
Waziri wa afya wa Afrika Kusini
Amesema kuwa zaidi ya asili mia 28% ya wasichana wa shule wameambukizwa
virusi vya Ukimwi, ikilinganishwa na asili mia 4% tu ya vijana wa shule.
Hii ameelezea ni kutokana na kuongezeka
kwa mababa sukari au kwa jina lingine, *fataki*, ( Wazee wanao tembea na
wasichana wadogo kwa umri).
Waziri
Aaron Motsoaledi amesema kuwa wamepata ushahidi kuwa wasichana wengi
wamejiingiza katika mapenzi na wazee waliowazidi ki umri badala ya kuwa
na vijana wa rika lao.
Madawa ya ARV
Takwimu za punde zaidi zimeonyesha kuwa asili
mia kumi ya raia wa Afrika Kusini wanaishi na virusi vya HIV. Nchi hiyo
imekuwa na mradi wa kuvuma zaidi wa kutoa dawa za kukabili makali ya
virusi hivyo vya HIV , ARV tangu rais Jacob Zuma alipomteua bwana
Motsoaledi kuongoza wizara hiyo ya afya yapata miaka minee iliyopita.
Related Product :
Why Shop on Bongo Online?
We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be
0 comments:
Post a Comment