Mtoto
Simon Mrope mwenye umri wa miaka 11 mkazi wa eneo la mahenge katika
manispaa ya Songea mkoani Ruvuma alilazimika kukatisha masomo yake ya
shule ya msingi akiwa darasa kwanza kutokana na mtoto huyo kusumbuliwa
na ugonjwa wa moyo .
Awali
tulitoa habari za mtoto huyu akiomba msaada lakini hadi sasa bado
hajapata msaada wowote ule wa kuweza kuokoa maisha yake. Nahivi sasa
hali ya mtoto huyu inazidi kuwa mbaya kiafya .
Mtoto
Simon Mrope alikubwa na ugonjwa huo wa moyo tangu mwaka 2001 mara baada
ya kuzaliwa na kugundulika kuwa moyo wake una tundu hali ambayo
inamsababishia mtoto huyo kuvuta pumzi kwa shida.
Mama
wa mtoto Simon Mrope anayeitwa AMINA ALLY anawaomba watanzania
kumsaidia mtoto wake fedha za matibabu Baada ya kuambiwa na madaktari
kuwa Simon anatakiwa kwenda nchini india kutibiwa,baada ya kupata rufaa
kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili mwaka 2006 huku familia yake ikiwa
haina uwezo kabisa.
Majirani
wa familia ya Simon nao wanasema kuwa mtoto huyo anahitaji msaada wa
haraka kwa kuwa hali yake sio nzuri na kuwaomba watanzania wamsaidie.
Kinachosikitisha
zaidi baba wa mtoto huyo anayejulikana kwa jina la MROPE ameondoka
nyumbani hapo tangu mwaka 2011 na hajulikani aliko kwa sasa, ingawa
mwanzoni alisema yuko nchini Msumbiji.
Kwa anayeguswa na tatizo hili na anataka kumsaidia SIMONI MROPE atumie simu namba
0752732290
Mtoto Simon Mrope anavyoonekana hivi sasa kutokana na maradhi ya moyo yanayomsumbua.
Mtoto Simon Mrope akiwa na Mama yake Mzazi atambulikae kwa jina la Amina Ally.
0 comments:
Post a Comment