Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, July 16, 2013

Ghasia zaendeleamjini Cairo Misri huku Watu 7 wakiripotiwa kuuwawa

Ghasia zimekuwa jambo la kila mara Misri tangu Morsi kuondolewa mamlakani

Watu saba wameuawa mjini Cairo usiku wa kuamkia leo kufuatia makabiliano makali kati ta wanajeshi wa serikali na wafuasi wa rais wa Misri aliyeondolewa madarakani, Mohamed Morsi.
Polisi walitumia vitoa machozi kuwatawanya na kuwasukuma nyuma waandamanaji hao ambao walikuwa wakiwarushia mawe huku wakiwa wamefunga barabara kuu inayoelekea kati kati mwa mji mkuu.
Ghasia hizo zimetokea huku naibu waziri wa mambo ya nje wa Marekani, William Burns akiwa ziarani nchini humo.
Waziri huyo amesema taifa hilo limepewa nafasi ya pili kurejesha utawala wa kidemokrasia.
Bwana Burn alifanya mashauriano na viongozi wa serikali ya mpito ya nchi hiyo, lakini viongozi wa chama cha Muslim Brotherhood, walisusia mkutano huo.
Awali mamia ya wafuasi wa kiongozi aliyepinduliwa Misri Mohamed Morsi wamepambana na vikosi vya usalama katikati mwa mji wa Cairo na kuwafyatulia waandamanaji hao gesi ya kutoa machozi.
Mapigano hayo yanajiri muda mfupi baada ya mjumbe mkuu wa Marekani William Burns kutoa wito kwa vikosi vya usalama kujizuia kwa kiwango kikubwa katika kukabiliana na maandamano hayo.
Makabiliano yalifanyika baada ya naibu waziri wa mambo ya nje wa Marekani anayezuru Misri, kuwataka maafisa wa usalama kuhakikisha kuwa wanajitahidi kutuliza ghasia wakati wakijizuia kufanya mauaji yoyote.
Burns alikutana na maafisa wa serikali inayoungwa mkono na majeshi.
Lakini chama cha Muslim Brotherhood kimesema haikina nia ya kukutana na waziri huyo.
Akizungumza baada ya kukutana na viongozi wa serikali mpya inayoungwa mkono na jeshi nchini, mjumbe huyo, William Burns, amesema Misri imepewa nafasi ya pili kufuatia kupinduliwa na jeshi Mohammed Morsi.
Alikutana na serikali inayoungwa mkono na jeshi nchini lakini Muslim Brotherhood, inasema haina mpango wa kukutana naye. Naibu rais wa tawi la kisiasa la chama cha Morsi, Muslim Brotherhood,Essam el-Erian, ametoa wito wa utulivu.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop