Welcome to our online store Portal

Template Information

Friday, September 20, 2013

BOKO HARAM YAENDESHA OPERESHENI ABUJA

Vikosi vya usalama nchini Nigeria, vinasema vimeshambuliwa na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la, Boko Haram, mjini Abuja. dakika 37 zilizopita

Vijana wanaotoa ulinzi kwa wenyeji dhidi ya Boko Haram
Vikosi vya usalama nchini Nigeria, visema kuwa vishambuliwa na wapiganaji wa kiisilamu , Boko Haram, mjini Abuja.
Vijana wanaotoa ulinzi kwa wenyeji dhidi ya Boko Haram










Vikosi hivyo vimesema kuwa watu kadhaa walijeruhiwa wakati wapiganaji hao walipowafiatulia risasi maafisa waliokuwa wanatafuta silaha haramu.
Mapigano haya yanakuja siku tatu baada ya shambulio lengine lililofanywa na watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Boko Haram katika jimbo la Borno.
Mwandishi wa azizicompdoc.blogspot.com katika eneo hilo anasema kuwa baadhi ya watu hawajulikani waliko na kuwa huenda zaidi ya watu miamoja waliuawa.
Katika siku tatu zilizopita wafanyikazi katika sekta ya afya wamekuwa wakiondoa miili ya watu waliofariki kwenye malori.

Afisa mmoja alisema kuwa alihesabu mili themanini na saba.
Lakini kuna uwezekano mkubwa kuwa miili zaidi inaweza kupatikana katika misitu na taarifa nyingine zinasema kuwa wapiganaji hao wanaodaiwa kuwa wa Boko Haram, waliwaua zaidi ya watu mia moja arobaini baada ya kuweka vizuizi vya barabarani na kuvalia magwanda ya jeshi wakijidai kuwa wanjeshi.
Jumanne shambulio karibu na Benisheik ni kati ya mabaya mno tangu hali ya hatari itangazwe Kaskazini Mashariki mwa Nigeria Mei.
Juhudi za kumaliza wapiganaji wa kiislamu zimefanya maeneo ya mijini kuwa salama lakini jeshi haliwezi kusema kuwa limeshinda vita kwani watu wanaoishi mashambani wamo katika hatari ya kushambuliwa.
Kwa sasa ni vigumu kupata habari kwani laini zote za simu zimekatwa katika juhudi za kuwasaidia wanajeshi kufaulu katika mpango wao.

Manusura wa mashambulio hayo yanayodaiwa kufanywa na Boko Haram wanasema kuwa wapiganaji hao walikuwa wamevalia sare za jeshi.
Waliwasili kwa magari , wakaweka vizuizi kati ya Maiduguri na Damaturu na wakaanza kuwaua watu.
Waliojaribu kukimbilia misituni walifuatwa na kupigwa risasi.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop