Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ameipangua Bodi ya
Wakurugenzi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kwa kuwaondoa wajumbe
sita kati ya wanane kwa lengo la kuondoa migongano isiyo na tija ndani
ya mamlaka hiyo.
Amewateua wajumbe wapya watatu na kusababisha iwe wajumbe watano ambao ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) na Mwakilishi wa wafanyakazi wa TPA ambao hakuwataja majina.
Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo iliyotolewa jana, wajumbe waliondolewa ni Julius Mamiro, John Ulanga, Caroline Kavishe, Dk. Hildebrand Shayo na Asha Nasoro.
Dk. Mwakyembe pia amekubali ombi maalum la Dk. Jabiri Kuwe Bakari ambaye pia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa e-Government, la kujitoa kwenye ujumbe ili aelekeze nguvu zake katika kuiimarisha taasisi yake ambayo huduma zake zitanufaisha idara na taasisi zote za Serikali ikiwamo TPA.
Katika mabadiliko hayo, Dk. Mwakyembe amewabakiza wajumbe wawili ambao ni Saidi Sauko na Jaffer Machano.
Amewateua wajumbe wapya watatu na kusababisha iwe wajumbe watano ambao ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) na Mwakilishi wa wafanyakazi wa TPA ambao hakuwataja majina.
Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo iliyotolewa jana, wajumbe waliondolewa ni Julius Mamiro, John Ulanga, Caroline Kavishe, Dk. Hildebrand Shayo na Asha Nasoro.
Dk. Mwakyembe pia amekubali ombi maalum la Dk. Jabiri Kuwe Bakari ambaye pia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa e-Government, la kujitoa kwenye ujumbe ili aelekeze nguvu zake katika kuiimarisha taasisi yake ambayo huduma zake zitanufaisha idara na taasisi zote za Serikali ikiwamo TPA.
Katika mabadiliko hayo, Dk. Mwakyembe amewabakiza wajumbe wawili ambao ni Saidi Sauko na Jaffer Machano.
0 comments:
Post a Comment