Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, September 17, 2013

KAMBI YA KIJESHI MAREKANI YASHAMBULIWA NA WATU 12 WAPOTEZA MAISHA

Aaron Alexis
Mtu aliyewaua watu 12 katika kambi ya kijeshi nchini Marekani na kisha mwenyewe kuuawa, katika makabiliano na polisi, ametajwa kuwa mwanajeshi wa zamaji wa jeshi la wanamaji.
Aaron Alexis, 34, kutoka Fort Worth, Texas, aliuawa na polisi baada ya kuvamia kambi hiyo na kuwaua watu kiholela , mjini Washington DC.
Watu wengine wanane walijeruhiwa kwenye uvamizi huo ulioanza mapema asubuhi mnamo Jumatatu.
Rais Barack Obama aliamuru bendera kupeperushwa nusu mlingoti katika Ikilu ya White House na Capitol Hill.
Alisema anaomboleza kwa sababu ya mauaji mengine ya halaiki na kulaani kitendo hicho cha uoga.
Haijulikani kwa nini Aaron Alexis aliamua kufanya shambulizi hilo na kuwaua watu kati ya umri wa miaka 46-73.
Awali polisi walichukua hatua baada ya ripoti za watu wengine kujihami wakishirikiana na Alexis, lakini baada ya msako mkali wakasema kuwa hakuna dalili kwamba Alexis alikuwa na wenzake..
Valerie Parlave wa shirika la ujasusi la FBI alisema kuwa Alexis, aliyekuwa ameajiriwa na mwanakandarasi aliyekuwa anafanya kazi kwenye mtandao wa internet wa FBI, alikuwa na pasi ya kuingia kwenye eneo hilo.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop