Welcome to our online store Portal

Template Information

Monday, September 30, 2013

MKUU WA SHIRIKA LA KIJASUSI LA KENYA MICHAEL GICHANGI AHOJIWA LEO

Mawaziri wa serikali walipokea taarifa kuhusu tisho la mashambulizi ya kigaidi kabla ya kundi la Al Shabaab kushambulia jengo la Westgate mjini Nairobi.
Kwa mujibu wa taarifa za kijasusi zilizofichuliwa, zilionyesha maelezo ya mipango ya mashambulizi hayo kufanyika Nairobi au mjini Mombasa.
Mawaziri wanne na mkuu wa majeshi walikuwa wamefahamishwa kuhusu tisho la kufanyika shambulizi la kigaidi.
Watu 67 walifariki na mamia kujeruhiwa katika shambulizi la kigaidi ambalo Al Shabaab walikiri kulifanya Septemba 21 mjini Nairobi.
Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la Daily Nation, mawaziri walipopewa taarifa za kati ta yarehe 13 na 20 kuhusu uwezekano wa kufanyika mashambulizi kadhaa ya kigaidi mjini Mombasa na Nairobi.
Onyo hizo zilitolewa kwa mara ya kwanza mnamo mwezi Januari kwa mujibu wa gazeti hilo na kwa mara nyingine kuanzia Septemba.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, serikali ya Israel pia ilitoa taarifa za kuonya kuwa huenda magaidi wakashambulia majengo yanayomilikiwa na raia wake kati ya tarehe 4 na 28 Septemba.
Daily Nation limeripoti kuwa taarifa za kijasusi zilionyesha kuwa viongozi wa al-Shabab walikuwa wameanza kulenga maeneo ya kushambulia ikiwemo Westgate na kanisa la Holy Family Basilica.
Kuna hofu idadi ya waliofariki huenda ikaongezeka.
Maafisa wa serikali wanaosemekana kupokea taarifa hizo ni pamoja na waziri wa fedha, Julius Rotich, waziri wa usalama Joseph Ole Lenku, waziri wa maswala ya kigeni, Amina Mohammed, waziri wa ulinzi Raychelle Omamo na mkuu wa majeshi Julius Karangi.
Mkuu wa shirika la ujasusi Michael Gichangi, anatarajiwa kuhojiwa na kamati ya bunge kuhusu usalama siku ya Jumatatu.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop