Welcome to our online store Portal

Template Information

Friday, October 25, 2013

SAKATA LA GESI MENGI AVUNJA UKIMYA

Dar es Salaam. Suala la gesi lilizua balaa jana wakati wa mkutano wa wadau wa sekta hiyo baada ya malumbano makali kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi na Mwenyekiti wa Mfuko wa Sekta Binafsi (TPSF), Dk Reginald Mengi.
Maswi na Mengi walitofautiana juu ya suala la nafasi ya wawekezaji wazawa kwenye sekta hiyo ya gesi katika kongamano la pili la wadau wa mafuta na gesi jana jijini Dar es Salaam.
Malumbano hayo yalichochewa zaidi na kauli iliyotolewa juzi na Waziri wa Nishani na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ambaye alisema kuwa wazawa wana uwezo mdogo wa kuwekeza katika sekta hiyo.
Mengi arusha kombora
Mengi ndiye aliyeanza mashambulizi pale alipotaka wazawa wapewe kipaumbele kwenye uvunaji wa mafuta na gesi.
“Tunaambiwa sisi hatuna fedha. Eti hela zetu ni kwa ajili ya kufanyia biashara ya matunda. Lakini tunayo ardhi, Tanzania siyo nchi maskini, gesi ni mtaji wetu, tuweke mkakati wa kugawana hii rasilimali,” alisema Mengi na kuongeza;
“Huku ni kuwa maskini wa fikra na tutakuja kuulizwa na Mwenyezi Mungu. Kama Serikali haina sera itauzaje rasilimali zetu kwa wageni? Tusingependa kuyazungumza haya hadharani, lakini tunasema tu. Mtu mwenye hekima pale wizarani wa kutusikiliza ni Maswi peke yake.” Mengi alisema anataka kuona Serikali ikitumia mfumo wa taifa la Nigeria kwa kutoa kipaumbele kwa wazawa.
“Mimi katika masuala ya uwekezaji kwa kweli `role model’ (kivutio) ni nchi ya Nigeria,” alisema Mengi.
Mwakilishi wa taasisi
za dini ashindilia
Baada ya Mengi kukaa, alisimama Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili na Haki za Jamii, Mchungaji William Mwamalanga alisema Serikali inatakiwa kukubaliana na hoja za Watanzania katika uwekezaji wa sekta hiyo.
Mchungaji Mwamalanga aliongeza kuwa huu siyo wakati wa kuendelea kuwaachia wawekezaji hatua zote katika rasilimali ya Tanzania.
“Lazima tujifunze kwa mataifa kama Nigeria, serikali yao imetoa nafasi ya mwananchi kusimamia, yaani mwekezaji akiingia lazima apitie kwa mwekezaji wa ndani kabla ya kufanya mazungumzo na serikali. Kwa nini tusifanye hivyo pia? “alihoji Mchungaji Mwamalanga.
Mbali na hilo Mchungaji Mwamalanga alisema Serikali inatakiwa kukiri dhambi ya kuingia mikataba bila kuwapo kwa sera ya gesi.
Maswi ajibu mapigo
Baada ya Mengi na wajumbe wengine kutoa maoni ya kuilaumu Serikali, Maswi alitakiwa kutoa maelezo ya Serikali kuhusiana na suala hilo.
Maswi alionyesha wazi alikuwa amepandwa na jazba kufuatia maoni ya kuiponda Serikali na hakuchelewa kuanza kuwakosoa Mengi na wadau wengine.
“Katika andiko letu tumeandika, nawahimiza mkalinunue, tumewagusia wazawa ambao watahusishwa katika ununuzi wa vitalu. Hakuna aliyesema kuwa sekta binafsi haitashirikishwa,” alisema Maswi huku akifoka.
Maswi alisema kuna mambo mengi ambayo Watanzania wanayo fursa ya kushiriki katika uwekezaji wa sekta hiyo na siyo kukaa majukwaani na kuzungumza kwa unafiki.
Aidha, aliongeza kuwa mpaka sasa hajaona kampuni yenye uwezo mkubwa hapa nchini katika ushiriki wa moja kwa moja katika uwekezaji wa sekta hiyo.
“Tusijidanganye kwa vikampuni vidogovidogo tulivyonavyo, tukadhani kama vinaweza kuingia kwenye ushindani wa moja kwa moja. Vikampuni vyenyewe vimejaa rushwa tu za kuhonga, hakuna lolote tuache ubabaishaji, “ alisema Maswi. Aliukosoa pia mtindo wa uwekezaji wa Nigeria ambao Mengi ameupendekeza:
“Mengi kaka yangu, hakuna suala la mjomba katika masuala ya uwekezaji. Huo mtindo wa Nigeria siyo mzuri, huwezi kuwapa watu wachache rasilimali wakati wengi wakiwa kwenye umaskini. Nigeria imejaa vurugu na hatuwezi kuichukulia kama mfano mzuri,” alisema Maswi na kuongeza:
“Jukumu letu kama wizara na kila ninapokutana na ninyi, nakutana kama Katibu Mkuu, siyo Maswi. Lengo letu ni kuwaeleza kinachoendelea na jinsi ya kuwawezesha wazawa.”
Akijibu hoja ya Mchungaji Mwamalanga, Maswi aliwataka viongozi hao kushirikiana na Serikali badala ya kuinyooshea kidole.

“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iko tayari kukutana na kundi lolote. Mkitaka tuonane, leteni barua tu. Tuko tayari na hatufichi kitu,” alisema na kuongeza: “Tatizo la nchi yetu watu ni kulalamika tu, fanyeni kazi... Mkitusaidia maaskofu, tutatoka hapa tulipo, siyo kutunyooshea tu vidole.
Maaskofu wenyewe wanakula rushwa, wanafanya vitu vya ajabu, mbona sisi hatuwanyooshei? Au tuwataje? Kwa sababu msione tu Serikali ni watu wabaya, `no, let’s work as a team’,” alisema Maswi.
Aliendelea kusisitiza kuwa fursa ya uwekezaji ipo kwa watu wote bila kujali wa ndani au wa nje.
“Hakuna mtu anayekuja hapa ambaye ni mjomba wenu. Sasa kama nyie mnakaa nyuma nyuma, hebu muwekeze basi.
Hivyo vitalu tumetoa, nani ametaka `document’ tumemkatalia? Watu wanakuja wanaleta hela, sasa tuzikatae?” Kuhusu sera na sheria ya gesi na mafuta, Maswi alisema sheria ipo ila sera itakamilika ifikapo Mei mwakani.
“Nawaahidi hadi mwisho wa mwaka huu tutakuwa na sera ya wazawa, hivyo nawaomba mshiriki kutoa maoni. Kama tunayo sheria tangu mwaka 1970 na 1980 tunataka nini tena? Tunataka sera au sheria? Nadhani sheria ni kubwa zaidi, huwezi kwenda kinyume na sheria. Hata hivyo, sera tunayo tangu Oktoba mwaka huu, lakini bado iko kwenye mchakato. Itakamilika ifikapo Mei, 2014,” alisema Maswi.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop