Welcome to our online store Portal

Template Information

Wednesday, October 2, 2013

TOLEO LA 2: WAJUA FUKUTO KUHUSU RASIMU YA KATIBA?

Lugha ya Taifa na lugha za alama
4.-(1) Lugha ya Taifa ya Jamhuri ya Muungano ni Kiswahili na
itatumika katika mawasiliano rasmi ya kitaifa na kiserikali.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), lugha ya
Kiingereza inaweza kutumika kuwa lugha rasmi ya mawasiliano ya
kiserikali pale itakapohitajika.
(3) Serikali itaweka mazingira yatakayowezesha kuwepo kwa
mawasiliano ya lugha mbadala zikiwemo lugha za alama na nukta nundu
kwenye sehemu muhimu za umma na katika vyombo vya habari
vinavyotangaza habari zake kitaifa kwa ajili ya watu wenye mahitaji
maalum.
‐ 4 ‐
Tunu za Taifa 5. Jamhuri ya Muungano itaenzi na kuzingatia Tunu za Taifa
zifuatazo:
(a) utu;
(b) uzalendo;
(c) uadilifu;
(d) umoja;
(e) uwazi;
(f) uwajibikaji; na
(g) lugha ya Taifa.
SEHEMU YA PILI
MAMLAKA YA WANANCHI, UTII NA HIFADHI YA KATIBA
Mamlaka ya
wananchi 6. Jamhuri ya Muungano ni nchi inayofuata misingi ya
demokrasia inayozingatia haki ya kijamii, na kwa hiyo:
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka za nchi, na Serikali
itapata madaraka na mamlaka yake kutoka kwa wananchi
ambao kwa umoja na ujumla wao wanaimiliki na kuipatia
Katiba hii uhalali;
(b) lengo kuu la Serikali litakuwa ni maendeleo na ustawi wa
wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi; na
(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali kwa
mujibu wa masharti ya Katiba hii.
Watu na
Serikali 7.-(1) Muundo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo
vyake, katika uendeshaji na utekelezaji wa shughuli zake utazingatia
azma ya kukuza umoja wa kitaifa na kudumisha heshima ya Taifa.
(2) Kwa madhumuni ya masharti ya Ibara ndogo (1), mamlaka
ya nchi na vyombo vyake vinawajibika kuelekeza sera na shughuli zake
zote kwa lengo la kuhakikisha kwamba:
(a) utu na haki nyingine zote za binadamu zinaheshimiwa na
kuthaminiwa;
(b) sheria za nchi zinasimamiwa na kutekelezwa;
(c) Serikali itahakikisha kuwa shughuli zinazofanywa
zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha kwamba
utajiri wa Taifa unaendelezwa, unahifadhiwa na
unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa jumla na
pia kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine;
(d) ardhi ikiwa rasilimali kuu na msingi wa Taifa, inalindwa,
inatunzwa na kutumiwa na wananchi wa Tanzania kwa
manufaa, maslahi na ustawi wa kizazi cha sasa na vizazi
vijavyo;
(e) maendeleo ya uchumi wa Taifa yanapangwa na kukuzwa
kwa ulinganifu na kwa pamoja na kwa namna ambayo
inawanufaisha wananchi wote;
(f) kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anafanya kazi,
na kazi maana yake ni shughuli yoyote ya halali
inayompatia mtu kipato chake;
Tufuatilie toleo lijalo kujua zaidi

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop