Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiongea mbele jopo la Marais wastaafu wa Afrika
kuhusu linaloongozwa na Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe Joaquim Chissano
anayefuatana na Rais Mstaafu wa Botswana Mhe Festus Mogae leo Novemba
25, 2013 Ikulu jijjini Dar es salaam. Mhe. Chissano, ambaye ni
mwenyekiti wa Jopo hilo pamoja na Mhe Mogae, walifika Ikulu kusikiliza
upande wa Tanzania kuhusu mgogoro wa mpaka na nchi ya Malawi, baada ya
kufanya hivyo hivi karibuni huko Blantyre.(PICHA NA IKULU).
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete leo asubuhi amefanya mazungumzo na Bibi Mary
Robinson, Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) katika
eneo la Maziwa Makuu.
Mazungumzo baina ya Rais
Kikwete na Bibi Robinson yamehusu maendeleo na hatua iliyofikiwa katika
mgogoro wa Mashariki mwa DRC – Congo na jitihada zinazofanywa za
kutekeleza mkataba wa amani ambapo Tanzania imetoa mchango mkubwa katika
jitihada hizo.
“Nakupongeza
kwa juhudi zako katika masuala ya amani katika nchi za Maziwa Makuu na
pia nakuomba uendelee kutoa mchango wako zaidi wa mambo gani muhimu ya
kuzingatia baadae. Bibi Robinson pia amempa salamu za rambirambi Rais
Kikwete pamoja na familia za wanajeshi waliopoteza maisha yao katika
harakati za kuleta amani huko mashariki mwa DRC Congo.
Bibi Robinson amemuomba
Rais Kikwete aendelee kutoa mchango wake kwenye juhudi za kuleta amani
nchini Congo baada ya kikosi cha UN kufanikiwa kuwaondoa waasi wa
kikundi cha M23 kutoka Mashariki mwa DRC – Congo.
Viongozi hawa
wamekubaliana kuwa ipo haja ya kuendeleza juhudi za kuleta amani DRC na
kuangalia jinsi ya kusonga mbele na kubainisha mahitaji na hatua zaidi
za kuchukua katika kuhakikisha amani na usalama vinapatikana na
hatimaye kujenga uchumi wa DRC.
Wakati huo huo Rais
Kikwete amekutana na Rais Mstaafu wa Msumbiji Mheshimiwa Joachim
Chissano ambaye ni msuluhishi wa mgogoro wa Mpaka Kati ya Tanzania na
Malawi katika Ziwa Nyasa. Rais Chissano na ujumbe wake upo nchini
kusikiliza hoja za Tanzania kuhusu mpaka wa Ziwa Nyasa ambapo Rais
Kikwete amewasilisha hoja zake kwao. Tayari msuluhishi huyo
ameshasikiliza hoja za Malawi ambapo inatarajiwa hoja za nchi zote mbili
hizi zitatafsiriwa na kuzingatiwa katika kutafuta suluhu ya mgogoro huo
wa Ziwa Nyasa.
0 comments:
Post a Comment