Welcome to our online store Portal

Template Information

Friday, November 29, 2013

KINANA ASEMA VIONGOZI WA VYAMA TUACHE UMANGIMEZA KTK VYAMA KAMA KWELI TUNAHITAJI DEMOKRASIA YA KWELI NCHINI (TUKUBALI KUKOSOLEWA)

 
170
Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana jioni ya jana, amefanya mkutano mkubwa wa hadhara mjini Tunduma, ambao umehudhuriwa na maelfu ya wananchi. Katika mkutano huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Mwaka, Kinana aliambatana na majenbe ya Chama cha Mapinduzi , Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro, Katika mkutano huo Kinana amesema wananchi kuikosoa CCM sio kosa kwani Chama hicho kimeingia mkataba na wananchi pale kilipopewa ridhaa ya kuongoza nchi ili kutekeleza ilani yake ya uchaguzi na ni haki ya mtu yeyote wakiwemo wapinzani ili kujua maendeleo yao, Amesema CCM haitakubali kuona ukiritimba na umangimeza wa baadhi ya watendaji Serikalini na unakwamisha maendeleo ya wananchi, ameongeza kuwa kazi ya CCM ni kutenda tu na kazi ya wapinzani ni kusema maneno tu.
2
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Mwaka mjini Tunduma.
3
Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro akisalimia maelefu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano huo.
4
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa amebebwa juujuu na wananchi waliohudhuria kwenye mkutano huo.
5
Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro akisakata muziki na wakina mama wana CCM kabla ya kuanza kwa mkutano huo.
6
Wananchi wakisakata muziki kabla ya kuanza kwa mkutano.
7
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisakata muziki na wananchi.
9
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na ujumbe wake akilekea katika eneo la mkutano.
10a
Msafara ukiwasili mjini Tunduma ukitokea wilayani Ileje.
11
Maelfu ya wananchi wakishangilia wakati Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kianana hayupo pichani alipokuwa akiwahutubia.
12
Hapa akisisitiza jambo kwa wananchi hao wakati akitoa hutuba yake.
13
Mzee wa kimila wa kabila la wanamwanga wilayani Momba Jubeki Chipansia akimpa silaha za kijadi Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana baada ya kumsimika kuwa miongoni mwa wazee wa kabila hilo katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Tunduma jana jioni.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop