IMG_0741
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto Ummy Mwalimu akizungumza katika Siku ya Maombi na Matendo kwa Watoto Duniani iliyoadhimisha jijini Dar es Salaam kwenye viwanja vya Don Bosco, Kulia kwa Waziri ni Naibu Mwakilishi wa UNICEF Paul Edward, Kushoto kwa Waziri ni Meneja wa GNRC Elizabeth Mwase na mbali kushoto ni Ofisa toka UNICEF.
.Utafiti umebaini kuwa kati ya watoto 10 watatu wamefanyiwa vitendo vya unyanyasaji


Serikali imekiri kuwa ukatili dhidi ya watoto ni changamoto kubwa kwani utafiti umebaini kati ya watoto 10 wa kike 3 wameshafanyiwa vitendo vya unyanyasaji wa kingono na kati ya watoto 7 wa kiume mmoja amesha fanyiwa vitendo vya unyanyasaji wa kingono au kimwili.
Akizungumza kwenye Siku ya Maombi na Matendo kwa Watoto Duniani (World Day of Prayer and Action for Children) Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto, Mhe Ummy Mwalimu amesema vitendo vya unyanyasi wa kingono na ukatili dhidi ya watoto ni changamoto kubwa kwa serikali, mashirika yasiyo kuwa ya kiserikali, jamii, wazazi, walezi na wananchi kwa ujumla.
“Cha kushangaza kuwa vitendo vya unyanyasi wa kingono au kimwili na ukatili dhidi ya watoto vinatendeka mashuleni na majumbani mahali ambapo watoto wanapaswa kuwa salama,” 

“Katika utafiti huo ilibainika kuwa karibu robo tatu ya wanaume na wanawake wamewahi kufanyiwa ukatili kabla ya umri wa miaka 18 na watu wazima au na jamaa zao wa karibu na robo moja wamesababishiwa na mtu mzima ukatili wa kifkra,” amesema Ummy Mwalimu.
IMG_0724
Naibu Waziri Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akizungumza na watoto wa shule mbalimbali za msingi na Sekondari.
Amesema ukatili dhidi ya Watoto na unyanyasaji wa kingono kwa watoto wa kike na kiume chini ya umri wa miaka 18 una athari kubwa katika siku za baadaye hasa katika Afya ya jamii husika.

Mwalimu aliendelea kusema kuwa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto imefungua kituo cha pamoja (One Stop Centre) katika hospitali ya amana jijini Dar es Salaam katika harakati za kusaidia waathirika wa vitendo vya kikatili na kingono.
Amesema serikali ya awamu ya nne inajipanga kuja na mkakati mfumo bora zaidi wa kuwalinda watoto wa kike na kiume dhidi ya vitendo vya unyanyasi wa kijinsia na ukatili dhidi yao.

Kwa Upande Meneja Mradi wa Mtandao wa Watoto na Vijana kutoka Imani Mbalimbali (GNRC) Bi, Elizabeth Mwase amesema pamoja na serikali kupitisha sheria ya kumlinda mtoto ya mwaka 2009 bado vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vinaongezeka.
Mwase amesema kuwa asasi za kiraia kwa kushirikiana na serikali wataendelea kuelimisha jamii umuhimu wa kuheshimu haki za watoto na kuboresha au kutunga sheria zinazomlinda mtoto mahali popote pale katika makuzi yake.
“jamii iliyolelewa katika mazingira mazuri ina nafasi kubwa ya kuleta matokeo chanya kwenye mustakabali wa taifa kwa ujumla lakini jamii iliyolelewa vibaya haiwezi kubadilisha taifa kwa sababu ni zao la tunda baya,” amesema.
IMG_0583
Naibu Mwakilishi wa Shirika la Umoja la Mataifa la Watoto (UNICEF) Paul Edward akisoma risala kwenye Siku ya Maombi na Matendo kwa Watoto Duniani iliyoadhimisha leo jijini Dar es Salaam kwenye viwanja vya Don Bosco.

Kwa upande wake Naibu Mwakilishi wa Shirika la Umoja la Mataifa la Watoto (UNICEF) Paul Edward amesema mwaka 1989 Umoja wa Mataifa iliweka mkataba wa siku ya kimataifa ya mtoto ili kutambua na kumlinda mtoto dhidi wa ukatili wa aina yeyote hapa duniani.
Amesema Umoja wa Mataifa, asasi za kirai na mashirika yote yasiyo ya kiserikali wanapaswa kuisaidia jamii na serikali katika kutokomeza ukatili dhidi ya watoto kwa sababu ni taifa la kesho.

IMG_0459
Meneja Mradi wa GNRC Elizabeth Mwase akitoa neno wakati wa maadhimisho hayo ya siku ya Maombi na Matendo kwa Watoto Duniani akiwa na baadhi ya wageni waalikwa meza kuu.
IMG_0519
Wanafunzi kutoka shule ya Msingi Kumbukumbu wakisoma risala ya watoto.
IMG_0364
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiteta jambo la Naibu Mwakilishi wa Shirika la Umoja la Mataifa la Watoto (UNICEF) Paul Edward.
IMG_0688
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia tukio hilo.
IMG_0877
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akicheza kwaito na wanafunzi wa shule za msingi jijini Dar.
IMG_0790