IMG_2355
Katibu Mkuu wa Zanzibar Association for Youth, Education and Empowerment, Fatma Mabrouk Khamis akizungumza na waandishi wa habari wakati wa semina hiyo ya ujasiriamali wa kuandika michanganuo ya kuandika biashara.

Watanzania wameombwa kuwa na utamaduni wa kujitokeza kwa wingi katika semina mbalimbali zinazolenga kuhamasisha na kufundisha ujasiriamali katika harakati za kupambana na tatizo la ajira nchini. MOblog inaripoti.
Akizungumza na Moblog jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Katibu Mkuu wa Zanzibar Association for Youth, Education and Empowerment, Fatma Mabrouk khamis amesema wao Jumuiya ya wanawake wa wajasirimali Tanzania kwa kushirikiana na taasisi ya Kinu waliandaa semina ya mbili ya jinsi ya kufundisha kuandika michanganuo ya kibiashara kwa wajasiriamali vijana nchini.

“Tumepata takribani vijana kumi na moja toka sehemu mbalimbali za mkoa wa Dar es Salaam na wamefundishwa jinsi ya kuandika michanganuo ya kibiashara na kuanza biashara kwa mtaji wa chini,” amesema Fatma.
Amesema kuwa washiriki wa semina walikuja na mawazo ya kuanzisha biashara mbalimbali kama kuhamasisha utalii wa ndani, biashara kwa mfumo wa teknonojia, biashara za kimataifa na kurasa zinaonyesha uainisho wa biashara na makampuni mbalimbali.
Bi. Khamis amesema kuwa katika Ujasiriamali kuna mbinu nyingi za kuweza kumfanya mjasiriamali kuweza kujitanua na kufanya biashara za ndani za kikanda na kimataifa endapo watakuwa wabunifu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Professional Approach Development (PAD) Lilian Secelela Madeje amesema kuwa kikundi chao kwa ksuhirikiana na taasisi ya kinu watashirikiana na taasisi za fedha kuelezea changamoto za upatikanaji wa mitaji katika kuanzisha biashara.
Madeje alisisitiza kuwa mjasiriamali unaanzia kwenye wazo ambalo baadaye linakuwa kwenye vitendo kupitia taasisi za fedha zenye kutoa mikopo kwa riba nafuu katika kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo wa watanzania.
IMG_2360
Lilian Secelela Madeje Mkurugenzi Mtendaji wa Professional Approach Development akisisitiza jambo wakati wa semina hiyo ya Wajasiriamali.
IMG_2348
Wajasirimali wakiwa katika vikundi wakiandaa michanganuo ya biashara mbalimbali wakati wa kipindi cha majaribio.
IMG_2346
IMG_2358