Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa nyumba za Walimu wa Shule ya Sekondari ya Mwakaleli.
Katibu
wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro akikata ubao
akiwa pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakikata
mbao kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya maabara na madarasa ya shule ya
Sekondari ya Mwakaleli.
Katibu
wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro akiongea na
wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Mwakaleli na kuwataka wanafunzi
waongeze bidii kwenye masomo kwani elimu haina mwisho.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu wanafunzi wa shule ya
sekondari ya Mwakaleli baada ya kumaliza kushiriki shughuli za
kimaendeleo ya ujenzi wa madarasa ,maabara na nyumbza za walimu.
Mbunge
wa Jimbo la Rungwe Magharibi Profesa David Mwakyusa akiwasalimu
wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mwakaleli na kuwataka
wajitahidikusona na kuepukana na vitendo vitakavyo waharibia maisha yao.
Wanafunzi
wa Kidato cha Sita wa shule ya Sekondari ya Mwakaleli wakiwa kwenye
picha ya pamoja na Katibu wa NEC Siasa na Mahusiano ya Kimataifa
Dk.Asha-Rose Migiro na Mbunge wa Viti maalum wanawake mkoa wa Mbeya
Dk.Mary Mwanjelwa.
Mzee
Issa Simion akitoa salaam kwa niaba ya wazee wa Kijiji cha Katende na
pia kushukuru kwa Serikali na Chama Cha mapinduzi na pia kuelezea kero
zinazohusu wakazi wa kata ya Katende.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kijiji cha
Katende ambapo alihimiza sana kuwa makini na vyama vinavyojita vya
siasa kwani sasa vimeanza kupoteza muelekeo.
Mbunge wa Wanawake Mkoa wa Mbeya Dk.Mary Mwanjelwa akiwasalimia wakazi Katende
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye picha ya pamoja na
wazee wa kijiji ambao leo walimpa heshima ya kuwa Mzee wa Katende na
kumvisha mgolole kama heshima ya mtu mzima.
Katibu
wa NEC Siasa na Mahusiano ya Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro akiwa
ameketi kwenye mkeka unaojulikana kama Kalili aliopewa zawadi na wakina
mama wa Katende.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Katende na
kuwaahidi CCM inatekeleza ilani yake ya uchaguzi na kusema ahadi
zilizoahidiwa zitatimizwa.
Katibu Mkuu wa CCM aliwaambia wananchi hao kuwa lazima tuhoji serikali pesa za maendeleo kwa nini haziji kwa wakati.
0 comments:
Post a Comment