Welcome to our online store Portal

Template Information

Sunday, November 17, 2013

WAZIRI MAGUFULI AUWASHA MOTO

Picha Na 1
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (mbele) akikagua moja na makalvati makubwa wakati alipofanya ziara ya kushtukiza kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa barabara ya Nzega hadi Puge mkoani Tabora.
Picha Na 2
Injinia Haile Tadase (aliyenyoosha mkono) kutoka Kampuni ya SMEC inayosimamia ujenzi wa mradi wa barabara ya Nzega – Puge akimpa maelezo Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (mwenye suti) wakati alipofanya ziara ya kushtukiza kukagua maendeleo ya mradu huo.
Picha Na 3
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wananchi wa mji wa Nzega waliojitokeza katika mkutano wa hadhara wakati alipofanya ziara ya kushtukiza kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa barabara ya Nzega hadi Puge mkoani Tabora.
Picha Na 4
Wananchi wakimsalimia Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (mwenye suti) mara baada ya kumaliza kuwa hutubia katika  mkutano uliofanyikia viwanja vya stendi mjini Nzega.

Mkandarasi anayejenga barabara inayotokea Nzega hadi Puge mkoani Tabora amejikuta matatani baada ya Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kufanya ziara ya kushtukiza kukagua maendeleo ya Mradi huo.
Mradi huo ambao ni sehemu ya barabara inayounganisha miji ya Tabora na Nzega, unajengwa na Mkandarasi  China Communications Construction Company Ltd (CCCC) kutoka Jamhuri ya Watu wa China. Kimkataba mkandarasi huyo alipaswa kuwa amekamilisha kazi hiyo mwezi Mei mwaka huu wa 2013 lakini hadi Waziri Magufuli anatembelea mradi huo kulikuwa na asilimia 30 tu ya kazi zilizokamilika.
Kwa mujibu wa Meneja wa Barabara mkoa wa Tabora Injia Damian Ndabalinze,  mradi huo ulisainiwa mwezi Julai 2010 ukiwa umepangwa kukamilika katika kipindi cha miezi 27.

Naye Meneja wa Kampuni ya CCCC inayojenga barabara hiyo Injinia Zhou Ming Tao, akijitetea kuhusu kuchelewa kukamilika kwa mradi huo alizitaja baadhi ya sababu zinazo sababisha mradi huo kusuasua kuwa ni tatizo la upatikanaji wa maji kwa ajili ya kazi za ujenzi pamoja na kusubiri kwa muda mrefu malipo kwa madai yao waliyowasilisha Tanroads.

Wakati akihutubia wananchi katika viwanja vya stendi mjini Nzega, Mheshimiwa Magufuli alizikataa hoja hizo na kumtaka mkandarasi huyo kuhakikisha kuwa anakamilisha kilomita zote 59 za mradi huo kwa kiwango cha lami ndani ya kipindi cha miezi 7 ijayo. “Nimefanya ziara ya kushtukiza na nimeona mkandarasi amekwishajenga makalvati na madaraja madogo 65 kati ya 68 hivyo kazi iliyobaki inaweza kukamilika ndani ya miezi saba endapo mkandarasi ataongeza kasi ya kazi na sitakuwa tayari kupokea visingizio vyovyote ambavyo vitasababisha ongezeko jingine la muda” alisisitiza Waziri Magufuli huku akimtahadharisha Msimamizi wa mradi huo kuhakikisha kuwa viwango vya ubora vinazingatiwa.

“Visingizio vya kutokuwepo kwa maji havikubaliki kwani mkandarasi alipata fursa ya kukagua mazingira ya mradi huo kabla ya kuwasilisha zabuni yake” alifafanua Waziri Magufuli na kuongeza kuwa hata hayo madai anayozungumzia mkandarasi ni visingizio visivyokubalika kwani kampuni yoyote inapoomba mradi mkubwa kama huo hutakiwa kuwa na mtaji wa kutosha.

Aidha, wakati akijibu maswali mbali mbali kutoka kwa wananchi, Mheshimiwa Magufuli aliwahakikishia wananchi hao kuwa ingawa barabara hiyo itapita nje kidogo mwa mji wa Nzega, pia kutakuwepo na barabara ya kiwango cha lami itakayounganisha barabara hiyo mpya na mji wa Nzega kwa kuifuata barabara inayotumika kwa sasa.
Wakiongea katika nyakati tofauti, Mheshimiwa Patrick Mbozu ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya pamoja na Bw. Abrahman Mndemi ambaye ni Mkurugenzi wa Hamashauri ya mji wa Nzega walielezea kuwa, kasi iliyoanza kuonekana katika siku za karibuni inatoa imani kuwa Mkandarasi huyo ataweza kuikamilisha kazi hiyo ndani ya kipindi hicho cha miezi saba kilichoelekezwa na Waziri wa Ujenzi.

Ujenzi wa barabara ya Nzega hadi Tabora umegawanywa katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza inaanzia Nzega hadi Puge na sehemu ya pili inatokea Puge kuelekea Tabora zote kwa pamoja zikiwa na urefu wa kilometa 114.5
Mheshimiwa Magufuli aliifanya ziara hiyo ya ghafla akitokea mikoa ya Mwanza na Geita alikokuwa akikagua shughuli mbali mbali za maendeleo.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop