Mjumbe
wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Balozi Seif Ali Iddi
akitoa salamu kwenye mkutano wa hadhara wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja
uliofanyika kwenye kiwanja cha michezo cha Mkaratini kilichopo ndani ya
Jimbo lake la Kitope.
Baadhi
ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakifuatilia matukio yaliyokuwepo
kwenye Mkutano wa Hadhara wa Wana CCM wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Hapo
Kitope ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa huo Haji
Juma Haji.
Wana
CCM walijikuta wakinengua wakati Kikundi cha burudani cha CCM Big Star
kikifanya vitu vyake kwenye mkutano wa hadhara wa CCM mkoa wa Kaskazini
Unguja uliofanyika kwenye kiwanja cha michezo cha Mkaratini kilichopo
ndani ya Jimbo lake la Kitope.
(Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ).
Wananchi
wa Majimbo ya Donge, Kitope na Bumbwini yaliyomo ndani ya Wilaya ya
Kaskazini “B” wameombwa kuitumia fursa na bahati waliyoipata ya uwepo wa
kiwanda cha Sukari Mahonda ambao utasaidia kwa kiasi kikubwa
upatikanaji wa nafasi za ajira wakati kitakapoanza rasmi kazi zake za
uzalishaji wa sukari.
Ombi
hilo limetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali
Iddi wakati akitoa salamu maalum kwenye Mkutano wa hadhara wa Wanachama
wa Chama cha Mapinduzi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja uliofanyika katika
uwanja wa michezo wa Mkaratini ndani ya Jimbo lake la Kitope.
Balozi
Seif amesema tabia ya baadhi ya watu kujaribu kufanya hujuma kwa
kuchoma moto mashamba yaliyooteshwa miwa ya kiwanda hicho inaweza
kuwafukuzisha wawekezaji ambao tayari wameshaonyesha nia ya kutaka
kuwekeza vitega uchumi vyao hapa Nchini.
Alieleza
kwamba wananchi wa Majimbo hayo wanapaswa kuwa makini pamoja na kukemea
vitendo hivyo viovu ambavyo endapo vitaachiliwa kuendelea kufanyika
katika maeneo hayo vitachangia kurejesha nyuma juhudi za Serikali kuu za
kukaribisha wawekezaji wanaopewa nafasi ya kuwekeza ili kusaidia uchumi
wa taifa pamoja na ustawi wa jamii.
“
Vitendo hivyo vinavyofanywa na baadhi ya wenzetu tunapaswa kuelewa
kwamba hatuwatendei haki wawekezaji wetu waliojitolea kuweka vitega
uchumi vyao hapa Nchini “. Alifafanua Balozi Seif.
Inasikitisha
kuona kuwa zaidi ya ekari kumi na nane zilizooteshwa miwa kwa ajili ya
usagaji wa sukari wakati utakapoanza uzalishaji tunaarifiwa kwamba
zimeteketea kwa moto unaosadikiwa kuwa ni hujuma za makusudi “.
Alionyesha Masikitiko yake Balozi Seif.
Aliwashauri
wananchi hao kuwa walinzi wa miradi ya uwekezaji ambayo mingi kati yao
huwanufaisha wananchi walioziunguukwa na miradi hiyo.
Akizungumzia
suala la siasa Balozi Seif ambae pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya
Halmshauri Kuu ya Taifa ya CCM na Mbunge wa Kitope aliwatahadharisha
wana CCM na wanachi wote Nchini kutokubali kudanganywa na baadhi ya
wanasiasa wenye sera zisizotekelezeka.
Amesema
wanachokihitaji wananchi walio wengi nchini ni sera pamoja na kile
wanachokihitaji kitekelezwe na Viongozi waliowachagua katika maeneo yao
na si vyenginevyo.
Alifahamisha
kwamba baadhi ya wanasiasa hivi sasa wamekuwa kero mitaani kwa tabia
yao ya kuendeleza matusi na lawama kiasi kwamba zinakwenda kinyume na
mfumo wa vyama vingi vya siasa lakini hata na maadili ya dini.
Aliwataka
wananchi kuendelea kuiamini Serikali yao yenye lengo la kuwaletea
maendeleo kwa kujenga miundo mbinu itayotoa fursa ya kutanuka kwa huduma
za Kiuchumi samba mba na kupunguza umaskini.
“
Tunapaswa tuangalie kwa makini tokea mapinduzi ya Zanzibar ya Mwaka 1964
hadi leo Bara bara ngapi zilizojengwa katika maeneo yetu. Sasa lazima
tuelewe kwamba Zanzibar ni ya Wazanzibari wenyewe na wao ndio
watakaohusika katika kuijenga “. Alisisitiza Balozi Seif.
Aidha
Balozi Seif alieleza kwamba lengo la Serikali zote mbili ile ya
Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na ya Mapinduzi ya Zanzibar ni
kuimarisha Muungao kwa faida ya watu wake wote.
Alifahamisha
kwamba cheche ya ubaguzi inayoendelezwa na baadhi ya watu kwa kutaka
kuvunja muungano haiwatendei haki Wazanzibari walio wengi wanaoishi
upande wa Bara wa Muungano.
Amesema
choko choko hizo zinaendelea kuchochewa wakati tayari wazanzibari hao
wameshawekeza miradi kadhaa ya kiuchumi inayoweza kusambaratika kama
fitina hiyo ikiachiliwa kuchomoza zaidi.
Mjumbe
huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi
alisisitiza na kuweka wazi kwamba msimamo wa Chama cha Mapinduzi uko
wazi wa mfumo wa Serikali mbili ambazo ndio muhimili wa kuendelea kuwepo
kwa Muungano uliopo hivi sasa.
0 comments:
Post a Comment