Rais
wa shirikisho la wachimbaji madini Tanzania (FEMATA), John Bina
akifungua kikao cha kwanza cha kamati ya dhahabu ya FEMATA Taifa,
kilichofanyikia mjini Singida.Wa kwanza kulia na mwenyekiti wa FEMATA
Ahmed Adamu na kushoto ni Golden Hainga, katibu wa FEMATA.
Katibu
wa chama cha wachimbaji madini mkoa wa Singida,Farijala Kiunsi akitoa
taarifa yake ya utekelezaji katika kikao cha FEMATA.
Baadhi
wa wajumbe wa mkutano wa FEMATA wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa
zikitolewa kwenye kikao cha wachimbaji Dhahabu mkoani Singida.
Rais
wa FEMATA Taifa, John Bina (wa pili kulia walioketi) akiwa kwenye picha
ya pomoja na viongozi wa kitaifa wa FEMATA taifa waliohudhuria kikao
mjini Singida.Wa kwanza kulia ni mwenyekiti wa FEMATA, Ahmed Adamu na
kushoto ni katibu wa FEMATA,Golden Hainga.(Picha zote na Nathaniel
Limu).
RAIS
wa Shirikisho la wachimbaji madini Tanzania (FEMATA), John Bina,
amewataka wachimbaji madini kujenga utamaduni wa kuwa na nidhamu ya
matumizi ya fedha ili fedha wanazozipata ziweze kuwaletea maendeleo
endelevu.
Bina
amesema hayo wakati akifungua kikao cha kamati ya dhahabu ya FEMATA
taifa, kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya madini kanda
ya kati mjini hapa.
Amesema
wachimbaji madini wamekuwa na sifa mbaya kwa madai kwamba, wengi
hutumia fedha vibaya na kupelekea shughuli ya madini kutokuwanufaisha
kimaisha.
Bina amesema matumizi hayo mabaya ya fedha, yana madhara mengi ikiwemo mhusika kufilisika mapema.
“Uzoefu
unaonyesha kwamba mchimbaji akipata kwa mfano shilingi milioni
10,kipaumbele chake kinakuwa ni kuoga mwili kwa pombe (bia), ataacha
kuchimba madini na kutumbukia kwenye anasa hadi hapo fedha
zitakapomwishia”,alifafanua Rais huyo.
Kwa
hali hiyo,Bina aliwataka wabadilike na kuwa na nidhamu nzuri ya
matumizi ya fedha, ili fedha wanazozipata ziwasaidie kujiletea maendeleo
wao binafsi,familia zao,mkoa wao na taifa kwa ujumla.
Katika
hatua nyingine, Rais Bina aliwataka wachimbaji madini kujiepusha na
uchimbaji haramu na pia wajenge utamaduni wa kulipa kodi, ili kujijengea
mazingira ya kukopesheka na taasisi za kifedha.
Wakti huo huo, kikao hicho kilimteua Farijala Kiunsi kuwa katibu wa FEMATA Taifa.
0 comments:
Post a Comment