Baadhi
ya Vijana wa CCM, wakibeba Jeneza lenye mwili wa marehemu Peter
Mangula, wakati wakiwasili kwenye makaburi ya Kinondoni kwa maziko.
(Picha na OMR).
Jeneza lenye mwili wa marehemu Peter Mangula likishushwa kaburini.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiweka udongo katika kaburi la mtoto wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara,
Philip Mangula, (Peter Mangula), wakati wa shughuli za maziko
zilizofanyika katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Makamu
Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula, akiweka udongo kwenye kaburi la
mtoto wake, Peter Mangula, wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika
katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam,
Watoto wa marehemu, wakiweka udongo kwenye kaburi ikiwa ni ishara ya kumzika baba yao.
Makamu
Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula, akiwaongoza sehemu ya
wanafamilia kuweka shada la maua kwenye kaburi la mtoto wake, (Peter
Mangula), wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika katika makaburi ya
Kinondoni.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiweka Shada la maua kwenye kaburi la mtoto wa Makamu Mwenyekiti wa
CCM Bara, Philip Mangula, (Peter Mangula), wakati wa shughuli za maziko
zilizofanyika katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Meya wa Ilala, Jerry Slaa,akiweka shada la maua.
Kingunge Ngambale Mwilu, akiweka shada la maua kwa niaba ya wazee.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dkt. Wilbload Slaa, akiweka Shada la maua.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Mwigulu Nchemba na Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, wakiweka mashada ya maua.
Waziri Mkuu Mstaafu, Salim Ahmed Salim,akiwaongoza mawaziri wenzake wastaafu, kuweka mashada ya maua.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akijumuika na waombolezaji wakati wa shughuli za maziko ya mtoto wa
Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula, (Peter Mangula) zilizofanyika
kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment