Mjumbe
wa Kamati Kuu ya CCM, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel
Nchimbi akizungumza na wanafunzi wa Vyuo Vikuu wa Umoja wa Vijana Mkoa
wa Morogoro. Waziri Nchimbi aliwasikiliza maoni yao pamoja na maswali
ambayo yalilenga kuimarisha chama chao mkoani humo. Kikao hicho
kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Mount Uluguru mjini
Morogoro. Picha na Felix Mwagara.
Mwanafunzi
wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) ambaye ni mwana CCM wa Umoja
wa Vijana wa Vyuo Vikuu mkoani Morogoro akimuuliza maswali ya
kuimarisha chama Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Waziri wa Mambo ya Ndani
ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (wapili kushoto-meza kuu). Waziri Nchimbi
aliwasikiliza maoni na maswali mbalimbali wanafunzi hao ambayo yalilenga
kuimarisha chama hicho mkoani humo. Kikao hicho kilifanyika katika
Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Mount Uluguru mjini Morogoro. Picha na
Felix Mwagara.
Mjumbe
wa Kamati Kuu ya CCM, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel
Nchimbi (Watatu kulia-waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na
wanafunzi wa Vyuo Vikuu wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Morogoro. Waziri
Nchimbi aliyasikiliza maoni pamoja na maswali yao ambayo yalilenga
kuimarisha chama chao mkoani humo. Kikao cha kuimarisha chama chao
kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Mount Uluguru mjini
Morogoro. Picha zote na Felix Mwagara.
0 comments:
Post a Comment