Welcome to our online store Portal

Template Information

Sunday, December 29, 2013

MTOTO WA MWAKA 1 AUAWA NA KUKATWA SEHEMU ZA SIRI

http://www.azizicompdoc.blogspot.com/
Watu saba wamefariki dunia katika matukio tofauti wakati wa   Sikukuu ya Krismasi mkoani Morogoro, akiwemo mtoto wa mwaka mmoja kuuawa na watu wasiofahamika kisha kukatwa sehemu zake za siri na mwili wake kutupwa pembezoni mwa Mto Morogoro.
 Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Faustine Shilogile alimtaja mtoto aliyefariki  kuwa ni James Stephen (1), mkazi wa Nanenane Manispaa ya Morogoro na kwamba tukio hilo lilitokea Desemba 25 mwaka huu saa moja asubuhi.
 Katika tukio la pili, mtoto Veronica Chigunda (6) mkazi wa Mashambani Likwambe, Wilaya Ulanga alifariki dunia wakati akipelekwa Hospitali ya Lugala baada ya kuungua moto wakati amelala kwenye nyumba anayoishi.
 Kamanda Shilogile alisema kuwa tukio hilo lilisababisha majeraha kwa watu wawili, akiwemo mama wa marehemu Paula Fimbo (24) na Matiasi Mahumba (1) na wote wamelazwa katika hospitali hiyo.
 Shilogile alisema tukio la nne, mfugaji wa jamii ya kimasai Mela Kipara (25) mkazi wa Makole wilayani Mvomero, alifariki dunia baada ya kukatwa na mapanga na mfugaji mwenzie wakati wakitoka kunywa pombe za kienyeji.
Aidha, Mganga Machaku (35) mkazi wa Mdudu, Kilosa alikutwa ndani ya nyumba yake amekufa na mwili wake ukiwa umeharibika vibaya huku chanzo cha kifo hicho kikiwa ni kunywa pombe za kienyeji kupita kiasi.
Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi  Kanda Maalumu  Dar es Salaam, limejipanga kuongeza  ulinzi katika kuelekea mkesha wa Mwaka Mpya.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop