Welcome to our online store Portal

Template Information

Sunday, December 29, 2013

WATU WANNE WAILUWA GEITA

http://www.azizicompdoc.blogspot.com/
Watu wanne wakazi wa Kijiji cha Nyankumbu mkoani Geita, wameuawa kikatili kwa kuchomwa moto na mwingine akifia kwenye dimbwi la maji kijijini hapo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa wa Polisi mkoani hapa, Leonard Paul alisema kuwa  tukio hilo la kikatili lilitokea usiku  wa juzi.
Paul alisema saa sita usiku watu wanaokadiriwa  watano walikwenda nyumbani kwa Mzee Barabara Luhemeja kwa lengo la kupora fedha .
“Watu hao walikwenda kwenye nyumba ya Luhemeja na kumkuta mtoto wake waliyemtaka kuwaonyesha mahali alipo baba yake,” alisema Kamanda Paul.
Alisema kuwa wakati wakiendelea kumhoji mtoto huyo awaonyeshe baba yake, ghafla alitokea ambapo watu hao walimweka chini ya ulinzi kabla ya kupora Sh60,000 ambazo ni rambirambi ya kufiwa na mjukuu wake.
Paul alisema kuwa baada kupora fedha hizo, walikimbia, ambapo mzee huyo alitoa kwa sungusungu walioanza msako wa watu haona kubahatika kumkamata mmoja aliyewataja wenzake.
Baada ya watuhumiwa wote kukamatwa, wananchi waliwafunga kamba na kuwachoma moto.
Akizungumza kwa huzuni, mama mmoja ambaye jina lake halikupatikana, ambaye pia miongoni wa waliouawa ni watoto wake, alisema: “Ndiyo kwanza napata taarifa kwamba watoto wangu walikuwa wezi,” Nyambona Malwa alisema kuwa hana taarifa.
Aidha Kamanda alisema kuwa watu waliouawa katika tukio hilo majina yao hayajafahamika, kwani walikuwa wageni kwenye kijiji hicho.
Kamanda Paul ameonya tabia ya wananchi kujichukulia sheria mikononi, kwani jeshi lake halitasita kuwachukulia hatua kali.
“Mpaka sasa tunawashikilia watu watatu kwa tuhuma za mauaji ya watu hayo na uchunguzi wa kuwabaini wengine unaendelea,” alisema Kamanda Paul.
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Said Magalula naye ameonya tabia ya wananchi kujichukulia sheria mikononi, akisema kamwe haivumiliki na kuwataka kuacha vitendo hivyo mara moja.
“Mwizi akikamatwa, asiuawe, wananchi watoe taarifa kituo cha polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe kama kupekwa kortini.”

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop